Ungependa kuifanya Kiswahili kuwa lugha ya chaguo lako, katika tovuti hii? |
Februari 12, 2013
Muungano wa vyama vitatu vya kisiasa nchini Djibouti vilifanya mikutano ya uchaguzi Jumapili na Jumatatu (tarehe 10 na 11 Februari), kuelekea kwenye chaguzi za wabunge zilizopangwa kufanyika tarehe 22 Februari.
Muungano wa upinzani wa Union for National Salvation (USN), ambao hapo zamani ulikuwa ukijulikana kama Holy Union for Change, ulifanya uchaguzi katika mji wa Balbala siku ya Jumapili, ukiongozwa na Ismail Gedi Hared, liliripoti Shirika la Habari la Djibouti. Huku wakizungukwa na wafuasi waliovaa rangi ya machungwa, wagombea wa USC walikariri shauku yao ya kuwepo kwa uchaguzi wa huru na haki. "Wakati wa wakubwa wanaokatalia mamlaka umekwisha na matakwa ya watu inapaswa kusimamia mabadiliko,' Hared alisema.
Pia siku ya Jumapili, llyas Moussa Dawaleh, kiongozi wa muungano wa chama kinachotawala cha Union for a Presidential Majority (UMP), aliwatangaza wagombea kwa wafuasi wa muungano huo waliokuwa wamevalia mavazi ya kijani karibu na uwanja wa Gouled, liliripoti gazeti la La Nation la Djibouti. Viongozi wa UMP waliwaomba wananchi wa Djibouti wasighiribiwe na ahadi za vyama vya upinzani. "Kutokana na sera zilizoundwa na Rais Ismail (Guelleh) na vyama ambavyo vinaunda muungano huu, nchi yetu sasa inaendelea, inapitia mageuzi na inajijenga yenyewe, na pia mustakabali wake wa baadaye una nuru", alisema Hassa Said Goumaneh, mmoja kati ya wagombea wakuu wa UPM.
Chama cha kisiasa za mrengo wa kati cha Centre for Unified Democrats (CDU) kilikutana na wafuasi wake katika uwanja wa Manispaa wa Falah Had siku ya Jumatatu, kikiongozwa na Omar Elmi Khaireh. Khaireh alitoa wito kwa wafuasi hao kupiga kura kwenye uchaguzi ujao, huku akibainisha changamoto za utawala wa sasa ikiwemo rushwa ambayo imetawala serikalini, upendeleo wa kindugu na upendeleo kwa jumla, ambayo alisema kuwa yote yanakwamisha maendeleo yakiuchumi ya Djibouti.
Kampeni za uchaguzi zilifunguliwa Ijumaa tarehe 8 Februari na zitaendelea kwa muda wa wiki mbili. Huu ni uchaguzi wa kwanza wa Djibouti ambao hautumii mfumo wa kushiriki vyama vikubwa pekee katika utawala, na unatarajiwa kutoa haki kwa vyama vidogo kuwa na sauti kubwa katika serikali.
Makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto, alisema kazi za Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia ...
Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia siku ya Alhamisi (tarehe 16 Mei) alipokea vyeti vya utambul...
Kwa uchache watu wanne waliuawa na watatu kujeruhiwa siku ya Alhamisi (tarehe 16 Mei) baada ya wa...
Kenya na Tanzania zilifanya operesheni ya pamoja ya ulinzi wa mpaka siku ya Alhamisi (tarehe 16 M...
Mwanachama wa kundi la wanamgambo wanaoiunga mkono serikali ya Somalia la Ahlu Sunna wal Jamaa, A...
Wanawake watatu waliuawa usiku wa Alhamisi (tarehe 16 Mei) katika eneo la Malkamau kwenye Kaunti ...
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon. siku ya Alhamisi (tarehe 16 Mei) alimteua waziri wa...
Tanzania na Canada zimesaini mkataba wa ushirikiano yanayokusudiwa kuimarisha na kuunda mazingira...
Jeshi la Taifa la Somalia liliwauwa wanamgambo 13 wa al-Shabaab siku ya Jumanne (tarehe 14 Mei), ...
Muda wa mwisho kwa wakaazi wa Mandera kusalimisha silaha zao haramu umeongezwa hadi Ijumaa (tareh...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji