Desemba 21, 2012
Kiasi cha watu 39 waliuawa katika mapigano mapya kati ya jamii za Pokomo na Orma katika eneo la Tana River Delta hapo Ijumaa (tarehe 21 Disemba), liliripoti shirika la habari la AFP.
Jamii hizo mbili zilipigana hivi karibuni katika majira ya kiangazi yaliyopita katika msururu wa uvamizi yalioua zaidi ya watu 100.
Ghasia za sasa zinaweza kuhusishwa na uchaguzi mkuu wa Kenya uliopangwa kufanyika mwezi Machi 2013, kwani mabadiliko ya mipaka ya wilaya yamepelekea kuondoka kwa nguvu za kisiasa kati ya makundi tafauti ya kikabila kwenye eneo hilo.
Polisi waliripotiwa kuiambia AFP kwamba mkasa huo wa hivi karibuni ulichangiwa na operesheni ya kuwanyang’anya watu silaha ambao ulishukiwa kulalia upande mmoja.
Picha zilizotumwa kwenye mtandao wa Twitter wa Msalaba Mwekundu zinaonesha viambaza vya mabanda yaliyovunjwa vikiwa vimesimama lakini mapaa yake yameteketezwa kabisa.
Shirika la Msalaba Mwekundu limesema kwamba timu lake la waokoaji lilikuwa likiwahudumia majeruhi, 30 kati yao wakiwa katika hali mbaya sana. Hawakutoa idadi kamili ya watu wote waliojeruhiwa.
Polisi nchini Tanzania wamewakamata watu 90 siku moja baada ya maandamano ambapo mtu mmoja aliuaw...
Kenya ililiomba Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa siku ya Alhamisi (tarehe 23 Mei) kufutwa kw...
Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia aliongoza sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya kuanzishwa ...
Mawaziri wa mambo ya nje wa mataifa wanachama wa Shirika la Maendeleo la Pembe ya Afrika (IGAD) w...
Kiongozi wa jamii huko Zanzibar, Mohammad Omar Said, alishambuliwa kwa tindikali siku ya Alhamisi...
Mahakama moja ya Puntland imewahukumu kifo watu saba kwa mauaji ya ulamaa wa Kisomali, Abdulkadir...
Shirika la kimataifa la misaada la Global Partnership for Education (GPE) limetangaza msaada wa d...
Shirika la kimataifa la kuteteta haki za binadamu la Amnesty International limetoa wito kwa Kenya...
Makamu wa Rais wa Kenya William Ruto ameahidi adhabu kali zaidi kwa majangili katika mswada wa Sh...
Raisi wa Kenya Uhuru Kenyatta siku ya Alhamisi (tarehe 23 Mei) alitoa majina mawili ya mwisho ya ...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji