Vijana wa Puntland wajiengua na al-Shabaab

Septemba 07, 2012

  • 1 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Sharmarke Abdi, mwenye umri wa miaka 18, na Said Omar, umri miaka 24, walijisalimisha kwa utawala wa mkoa wa Puntalnd hapo Alhamisi (tarehe 6 Septemba) baada ya kutoroka kutoka milima ya Galgala, maficho ya al-Shabaab.

  • Sharmarke Abdi, miaka 18, na Said Omar, miaka 24, waliachana na kundi la al-Shabaab na kujisalimisha kwa viongozi wa mkoa wa Puntland. (Hassan Muse Hussein/Sabahi).

    Sharmarke Abdi, miaka 18, na Said Omar, miaka 24, waliachana na kundi la al-Shabaab na kujisalimisha kwa viongozi wa mkoa wa Puntland. (Hassan Muse Hussein/Sabahi).

"Hivi karibuni, wote maafisa na wanajeshi wamekuwa wakijisalimisha kwa utawala walipong'amua kwamba wanadhoofika katika mikoa ya kusini mwa nchi kwa sababu ya kupoteza ngome zao," Naibu Waziri wa Usalama Abdi Jamal Osman Mohamed aliiambia Sabahi.

Alisema kuwashikilia vijana hawa kwa muda mrefu katika maeneo ya milima kumehatarisha mustakabali wao.

"Ukubalifu wa mawakala wa usalama kwa uasi wa watu hawa unafuatia utekelezwaji wa msamaha wa kirais wa Puntland kwa vijana wanaoondoka al-Shabaab, ukiacha majina makubwa yaliyotajwa na jumuiya ya kimataifa," alisema Mohamed.

Vijana hao waliopotoshwa walisema walikuako kwenye milima ya Galgala kwa miezi 13, alisema. Utawala wa Puntland uliwaonesha vijana hao wawili kwa vyombo vya habari siku ya Alhamisi.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 6)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • jeremiah jeremy
    September 7, 2012 @ 07:29:35PM

    Vijana waliobakia wanapaswa kufuata mfano huu MZURI na kujisalimisha kabla KDF haijawakamata.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo