Wanajeshi 2 wa Kenya waliopotea wahofiwa kufa

Septemba 06, 2012

  • 6 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Wanajeshi wawili wa Kenya ambao ni kati ya watu watano waliopotea wiki iliyopita baada ya kukamatwa kwa mji wa Miido kutoka kwa al-Shabaab wanahofiwa kuwa wamekufa, liliripoti gazeti la The Standard la Kenya hapo Alhamisi (tarehe 6 Septemba).

Msemaji wa Jeshi la Kenya Kanali Cyrus Oguna alisema kuna uwezekano mkubwa kuwa wanajeshi hao wawili walipelekwa Kismayo na al-Shabaab. Miili ya wanajeshi wengine watatu yalipatikana, alisema.

Al-Shabaab ilituma picha za wanajeshi waliouawa katika ukurasa wake wa Twitter wiki iliyopita kufuatia mapigano kati ya vikosi via Umoja wa Afrika na Somalia, ikidai kuwa marehemu hao walikuwa wanajeshi wa Kenya. Oguna hakuthibitisha ikiwa wanajeshi waliopotea ni miongoni mwa wale waliomo kwenye picha hizo.

Oguna alilaani utumwaji wa picha hizo, akisema ni ushahidi zaidi unaothibitisha jitihada za Kenya kuwaondoa al-Shabaab nchini Somalia zina thamani. "Hii ni ishara ya wazi na sura ya kikatili ya al-Shabaab na umbali tabia yao ya kinyama unavyoweza kufikia," alisema.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 10)

Dislike_icon(4)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • kenyan
    September 8, 2012 @ 09:45:13AM

    KDF wanapaswa kuwamaliza wahuni hawa mara moja kabisa kabisa, pamoja na kumaliza watu wabaya wachache (wafuasi wa al-Shabaab) nchini Kenya.

  • RICHARD MUGO
    September 8, 2012 @ 04:32:43AM

    Alshabab ni vazi la mapepo ambayo lazima yafutwe kutoka uso mzuri wa dunia. Tendo la kuburuza maiti wa mashujaa wetu waliokufa ni uhuni wa kishetani. Hakuna watu wanaomuogopa Mungu wangefanya vitendo hivyo vichafu. Washenzi hawa lazima waangamizwe hata kwa njia ya nyuklia. Wale walio na silaha kama hizo, wazitumie dhidi ya washenzi hawa. Tunahitaji kuiona Kismayu nzima ikiwaka kwa mionzi ya nyuklia na wale ambao watakamatwa lazima wafe kwa njia ya kifo cha maumivu zaidi na cha taratibu, wanapaswa kuburuzwa kwa kifo na miili yao kuchomwa moto.

  • Ambrose Korir
    September 7, 2012 @ 08:59:13AM

    Wakenya, tuwaombee Wakenya wenzetu walioko katika uwanja wa vita. Familia zao na marafiki wanakuwa hawalali usiku juu ya hili. Tuheshimu maiti na kufikiria mateso ya jamaa zao. Kumbukeni maneno ya msemaji wa KDF katika kutuma picha za mauaji yasiyothibitishwa.

  • Johnsonsilas,from Nairobi
    September 7, 2012 @ 03:21:50AM

    Hii inaweza kuwa bahati mbaya kwa sababu binamu yangu ni mmoja kati ya askari wawili waliopotea. KDF wametuhakikishia kuwa bado wanaendelea kutafuta wako wapi. Kwa sasa tunaweza kuomba tu kila kitu kiwe salama.

  • Isaac kiprono
    September 7, 2012 @ 02:39:17AM

    Naam, katika kutafuta amani, wahanga ni watatu waliofariki katika kuwalinda kaka na dada zao. Hongera wanaume na wanawake katika sare.

  • aadan
    September 7, 2012 @ 01:56:45AM

    Wanapaswa kuuliwa. Ni kitu gani kiliwaleta kutoka nchini kwao? Wamekosea sana.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo

Nyenzo