Agosti 28, 2012
Mamlaka ya Chakula na Madawa Tanzania (TFDA) imepanua matumizi ya teknolojia ya nyuklia ili kusimamia na kuboresha usalama wa chakula nchini, gazeti la Tanzania la The Citizen liliripoti.
TFDA imeweka kifaa maalumu cha maabara ili kugundua na kuchambua viharibifu vya metali, mabaki ya dawa zaa kuulia wadudu na vijisumu katika mazao ya chakula.
"Tunaatekeleza mkakati kazi wetu mpya wa miaka mitano kutoka 2012 hadi 2017," alisema Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Hitti Sillo katika uzinduzi wa mpango huo huko Dar es Salaam siku ya Jumapili (tarehe 26 Agosti). "Miongoni mwa malengo ya mpango huu ni kuipatia vifaa maabara ili kuchambua dawa za mifugo na mabaki ya dawa za kuulia wadudu ifikapo mwezi Juni 2015."
Mpango huu unasaidiwa na Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki, ambalo lilitoa shilingi milioni 345 million shillings (dola 220,000) kwa mradi huu, pamoja na vifaa vya maabara vyenye thamani ya kiasi cha shiilingi milioni 86 (dola 55,000).
Kaimu afisa mkuu wa afya Donald Mmbando alisema awamu ya kwanza wa mpango wa ulinzi wa chakula kwa kutumia nyuklia, ulioanza mwaka 2007 hadi 2010 iliongeza usalama wa chakula Tanzania, kwa vile bidhaa za chakula kilichoagizwa zilizoonekana kuwa na vichafuzi na vijisumu vilikataliwa kuingia nchini.
"Kusimamia vyakula vinavyoingia katika masoko yetu ni kitu ambacho hakiwezi kudharauliwa katika ulimwengu wa leo. ambao umekuwa kama kijiji cha dunia kukiwa na mzunguko huru wa bidhaa," alisema.
Raisi wa Kenya Uhuru Kenyatta siku ya Alhamisi (tarehe 23 Mei) alitoa majina mawili ya mwisho ya ...
Watu watano waliuawa na wanne kujeruhiwa katika mashambulizi mawili kwenye eneo la kaskazini mash...
Sababu kuu ya vurugu ambazo ziliua zaidi ya watu 150 katika Delta ya Mto Tana mwaka jana ilitokan...
Shirika la Afya Duniani (WHO) lilitangaza mlipuko wa polio katika Pembe ya Afrika siku ya Jumatan...
Majeshi ya serikali ya Somalia yamezifungia kampuni za mawasiliano ya simu na biashara nyingine h...
Serikali ya Somalia itaanza kuunda tawala za kikanda katika maeneo yaliyokombolewa kutoka kwa al-...
Waziri wa Nishati wa Djibouti Ali Yacoub Mohamoud na Balozi wa Japani nchini Djibouti Atsushi Nis...
Ufunguzi wa Mkutano wa Wasambazaji wa mafuta na gesi Tanzania utafanyika huko Dar es Salaam tareh...
Wabunge wameondoa hoja yao inayomtaka Waziri Mkuu Abdi Farah Shirdon na baraza lake la mawaziri k...
Rais Ahmed Silanyo wa mkoa wa Somaliland alikutana na Mwakilishi Maalum wa Umoja wa Ulaya kwa Som...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji
Maoni ya msomaji
UKIANGALIA THAMANI YA VIFAA TULIOPEWA MSAADA NA SHIRIKA LA ATOMIKI SERIKALI INAUWEZO WA KUGALAMIA,ILA 2MEISHA ZOEA MISAADA KUTOKA NJE.TUNASHUKURU ILA ISIWE KWA KUWA WAMEGUNDUA URANIAM KWETU WAKAANZA KU2NYONYA.WAJALI MASLAHI YA WANANCHI