Red_arrow

Ungependa kuifanya Kiswahili kuwa lugha ya chaguo lako, katika tovuti hii? |

Puntland na Galmudug zaapa kuongeza ushirikiano wa kiusalama

Agosti 28, 2012

  • 1 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Wawakilishi kutoka Puntland na Galmudug walikutana katika kituo cha polisi huko Galmudug siku ya Jumatatu (tarehe 27 Agosti) ili kuimarisha ushirikiano wa kiusalama baina ya tawala hizo mbili, mtandao wa Somalia wa Garowe Online uliripoti

"Puntland na Galmudug zilikutana kujadili hatima na hatua kuondokana na yaliyopita; tumedhamiria kufanyakazi pamoja ili kujenga usalama katika eneo hili," alisema Gavana wa Mudug, Mohamed Yusuf Jama.

Mkutano uliitishwa baada ya wizi wa gari kaskazini ya Galkayo, ulioripotiwa na polisi wa Puntland. Polisi ya Galmudug iliipata gari hiyo na kuirejesha kwa mwenyewe.

"Nataka kuwashukuru wawakilishi wa Puntland waliotutembelea na pia ninataka kuipongeza polisi wa Galmudug kwa kazi yao nzuri sana," alisema Makamu Gavana wa Galmudug Aweys Ali Saeed. "Naamini kuwa ikiwa tutafanya kazi pamoja tunaweza kuimarisha sana usalama katika eneo hili."

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 1)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • lugendo.R.H
    August 29, 2012 @ 07:16:54AM

    UMOJA NI NGUVU,UTENGANO NI DHAIFU.USHILIKIANO UNAFAIDA.HONGERA KWA HILO.GOOD IDEA

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo

Nyenzo