Agosti 28, 2012
Djibouti inapanga kujenga kiwanda cha kuzalisha umeme wa upepo chenye thamani ya faranga bilioni 18 (dola milioni 100) na kiwanda cha kusafishia maji katika bandari ya Doraleh, liliripoti gazeti la La Nation la Djibouti hapo Jumatatu (tarehe 27 Agosti).
Kiwanda hicho cha maji kitatoa ujazo wa mita 45,000 za maji safi kila siku, na utafiti unatabiri kwamba kinu cha umeme wa upepo kitatoa megawati 20 kwa siku.
Mradi huo unakusudiwa kumaliza upungufu wa maji ya kunywa nchini humo, hasa kwa wakaazi 820,000 wa mji mkuu. Serikali inatarajia kinu cha umeme wa upepo kupunguza gharama za kusafishia maji, na kuruhusu utoaji wa maji kwa gharama nafuu kwa watumiaji.
Mfuko wa Maendeleo wa Umoja wa Ulaya umeahidi msaada wa faranga bilioni 4.4 (dola milioni 25) kwa mradi huo na Shirika la Maendeleo la Pembe ya Afrika (IGAD) limeahidi msaada wa kati ya faranga bilioni 6.6 na bilioni 9.9 (kati ya dola milioni 38 na milioni 56) wa Djibouti chini ya mpango wake wa nishati endelevu.
Serikali ya Djibouti itafanya jitihada za kupatikana kwa sehemu iliyobakia ya fedha hizo, liliripoti gazeti hilo rasmi la serikali.
Ujumbe kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya Pembe ya Afrika (IGAD) uliwatembelea maafisa mjini Mogadish...
Mshukiwa wa ugaidi na mke wake walipigwa risasi na kufa na maafisa sita wa polisi walijeruhiwa wa...
Watu watano walikamatwa siku ya Jumanne mjini Dar es Salaam wakiwa na vifaa vya kulipua katika mi...
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta aliwataka wabunge kuweka kando madai yao ya kuongezwa mishahara kwa ...
Majeshi ya serikali ya Somalia waliwaua wanamgambo tisa wa al-Shabaab wakati wa mapambanao hapo J...
Mtu asiyejulikana alimpiga kwa risasi na kumuua ofisa wa kitengo cha usalama cha kijeshi huko kas...
Muungano wa Jubilee tawala cha Kenya kilichukua uongozi wa kamati mbili muhimu za bunge Ijumaa (t...
Chama cha Wafanyabiashara na Asasi ya Chakula na Kilimo ya Umoja wa Mataifa vinatoa mafunzo kwa w...
Balozi wa Umoja wa nchi za Ulaya nchini Tanzania Filiberto Ceriani Sebregondi aliwahamiza waandis...
Makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto, alisema kazi za Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia ...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji