Agosti 28, 2012
Waandamanaji walipambana na polisi katika mji wa bandari ya Kenya, Mombasa, kwa siku ya pili hapo Jumanne (tarehe 28 Agosti) baada ya mauaji ya Aboud Rogo Mohammed , mhubiri wa Kiislamu wa Kenya aliyefungamanishwa na al-Shabaab, liliripoti shirika la habari la AFP.
Wafanyakazi katika hospitali kuu ya Mombasa waliripoti kwamba kiasi ya watu 14 walijeruhiwa katika mapambano hayo, wakiwamo askari wawili wa kutuliza ghasia.
Mamia ya vijana wenye hasira waliyashambulia makanisa, kurusha mawe, kuharibu magari, kuzishambulia biashara na kupiga mayowe ya kumuunga mkono Rogo huku polisi wakijaribu kuwadhibiti.
"Tunajaribu kuwadhibiti ili tusisababishe vifo zaidi. Vifo na uharibifu wa mali hautasaidia chochote," alisema mkuu wa polisi wa mkoa huo, Aggrey Adoli.
Polisi wa Kenya walitumia mabomu ya machozi na kurusha risasi za mpira kuwazuia waandamanaji na kuwakamata watu 12 siku ya Jumanne, liliripoti gazeti la Daily Nation la Kenya.
Baraza Kuu la Waislamu la Kenya (SUPKEM) na jumuiya kadhaa za Kiislamu zimelaani ghasia hizo, hasa kuyalenga makanisa, ambapo matano kati yao yamechomwa moto.
"Ghasia kama hizi ni kinyume na imani yetu. Waandamanaji wasijifiche nyuma ya Uislamu au aina yoyote ya mafunzo yake," alisema Katibu Mkuu wa SUPKEM Adan Wachu, kwa mujibu wa AFP. "Hawa ni wahalifu na wachukuliwe hivyo."
Waziri Mkuu wa Kenya, Raila Odinga, alilaani mauaji dhidi ya Rogo, akiongeza kwamba serikali "imejitolea kuwafikisha wahusika mbele ya sheria."
Rogo alikuwa "kiongozi mkuu wa kiitikadi" wa kundi la Hijra nchini Kenya, ambalo pia hujulikana kama Kituo cha Vijana wa Kiislamu (MYC), kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa. MYC inaonekana kama mshirika wa karibu wa al-Shabaab nchini Kenya .
Kutokana na mauaji hayo, al-Shabaab iliwatolea wito Waislamu wa Kenya "kuchukuwa hatua zote muhimu" kuilinda dini yao.
"Waislamu wanapaswa kulichukulia jambo hili mikononi mwao, waungane dhidi ya makafiri na kuchukua hatua zote muhimu kuilinda dini yao, heshima yao, mali zao na maisha yao dhidi ya maadui wa Uislamu," ilisema taarifa ya al-Shabaab.
Raisi wa Kenya Uhuru Kenyatta siku ya Alhamisi (tarehe 23 Mei) alitoa majina mawili ya mwisho ya ...
Watu watano waliuawa na wanne kujeruhiwa katika mashambulizi mawili kwenye eneo la kaskazini mash...
Sababu kuu ya vurugu ambazo ziliua zaidi ya watu 150 katika Delta ya Mto Tana mwaka jana ilitokan...
Shirika la Afya Duniani (WHO) lilitangaza mlipuko wa polio katika Pembe ya Afrika siku ya Jumatan...
Majeshi ya serikali ya Somalia yamezifungia kampuni za mawasiliano ya simu na biashara nyingine h...
Serikali ya Somalia itaanza kuunda tawala za kikanda katika maeneo yaliyokombolewa kutoka kwa al-...
Waziri wa Nishati wa Djibouti Ali Yacoub Mohamoud na Balozi wa Japani nchini Djibouti Atsushi Nis...
Ufunguzi wa Mkutano wa Wasambazaji wa mafuta na gesi Tanzania utafanyika huko Dar es Salaam tareh...
Wabunge wameondoa hoja yao inayomtaka Waziri Mkuu Abdi Farah Shirdon na baraza lake la mawaziri k...
Rais Ahmed Silanyo wa mkoa wa Somaliland alikutana na Mwakilishi Maalum wa Umoja wa Ulaya kwa Som...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji
Maoni ya msomaji
vitendo kama hivyo serikali inapaswa kuwatia vijana wote mbaroni watakao patikana wakishirili katika visa hivyo kwene wengi wao ni wale hawana kazi zakufanya.
Daima huwa ninashangaa sana pale, anauawa mtu moja alafu makanisa, mabaa yanashamuliwa, hapo ninapata wasiwasi kuwa bado hatuna umoja kama waafrica. Bali tunakuwa watu wa kuongozwa na matukio
Ni pahali pazuri pa kujifunza masuala ya kikanda.
Nimehamaki sana. Ama vijana hawa wa Kiislamu wanaamini kwamba wengine sio vijana kwa sababu tu wao sio Waislamu au hawapati mafundisho sahihi popote pale wanapopata darasa za Kiislamu. Hatuko vitani nao na ninasema kwa ufupi tu watoke Kenya waende kufanya vita huko ambako wanaishi kwa kumwaga damu. Hasira kwa walengwa wasiohusika ni hasara kubwa kwa watu wasio na hatia.