Viongozi wa Kenya waidhinisha programu 5 za diploma kwa polisi

Agosti 19, 2012

  • 1 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Wizara ya Elimu ya Juu ya Kenya iliidhinisha siku ya Ijumaa (tarehe 17 Agosti) shule tano za mafunzo ya polisi ya diploma, gazeti la The Standard la Kenya liliripoti.

Fursa zilizopanuliwa kwa elimu ya polisi nchini Kenya ni sehemu ya jitihada za Kamati ya Utekelezaji wa Mabadiliko ya Polisi kuboresha huduma kwa umma, na zitatolewa huko Kiganjo, Embakasi, Utawala, Emali na Nairobi. Programu zitakuwa wazi kwa maofisa wa polisi waliopo na raia waliohitimu.

Kupitia makubaliano na Chuo Kikuu cha Kenyatta, Chuo cha Polisi cha Kenya kitatoa elimu ya kuwawezesha maofisa kuongeza sifa za taaluma zao, ambazo kabla ya hapo walizilitafuta nje ya jeshi kwa gharama zao.

Kamati ya polisi pia hivi karibuni iliwasilisha mtaala mpya kwa ajili ya mafunzo ya polisi ambayo yanalenga haki za kibinadamu, jinsia, mawasiliano na uhusiano na umma, maadili na miiko, huduma na kumjali mteja.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 2)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • muchirih
    August 20, 2012 @ 03:42:07PM

    Oooh Polisi wa Kenya. Kwa vyovyote vile, hili ni jeshi ambalo limejaa aibu kwa ufisadi sugu. Ni aibu...Aibu....Aibu...Polisi anapewa sare ya buluu kwa utambulisho rahisi wa kujipatia shilingi 50 kwa nguvu. Katika safari zangu husikia kichefuchefu ninapoona kundi la maofisa wa polisi katika vizuizi vya barabarani wakibadilishana mikono ya ufisadi na waendesha magari. Kuna tofauti ndogo baina ya polisi hawa wa vizuizi vya barabarani na al-Shabaab wa Somalia. Operesheni Linda Nchi malizeni kazi yenu haraka mje kuanzisha Operesheni Linda Nchi wamalize kazi yao kwa haraka na waingie kwa operesheni Linada wenye magari dhidi ya al-Shabaab hawa katika vizuizi vya barabarani zetu ili kuifanya trafiki yetu iwe ya kistaarabu.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo