Agosti 17, 2012
Kenya inatarajia kupata shilingi bilioni 100 (dola bilioni 1.2) za mapato kutoka sekta ya utalii mwaka huu, Waziri wa Utalii wa Kenya Dan Mwazo alisema siku ya Alhamisi (tarehe 16 Agosti).
"Ikilinganishwa na mwaka jana ambapo nchi ilipata shilingi bilioni 98 (dola blioni 1.1) kutokana na utalii, mwaka huu tunatarajia kupata shilingi bilioni 100," Mwazo alisema wakati kwa kutembelea Mbuga ya Taifa ya Maasai Mara, gazeti la Kenya la The Standard liliripoti.
Ongezeko lingeweza kuwa kubwa zaidi kama sio kwa matokeo ya karibuni ya ugaidi nchini Kenya, Mwazo alisema.
Mwazo alisema alitarajia idadi ya watalii wanaokuja Kenya itaongezeka kwa sababu ya mkazo wa serikali katika kampeni za kuitangaza. "Tumefanikiwa kuitangaza kama mahali pazuri zaidi ulimwenguni pa mafikio ya watalii, lakini masuala ya usalama na mtandao mbaya wa barabara vimetishia kurejesha nyuma mapato yetu," alisema.
Aliongeza kuwa ongezeko la mapato yanaweza kupatikana kupitia juhudi za kupanua matangazo mbali zaidi ya masoko ya kawaida ya utalii ya Kenya ya Uingereza, Marekani, Ujerumani, Ufaransa na Asia. "Kutegemea kupita kiasi masoko ya kawaida hakutaongoza mapato ya utalii," alisema.
Wizara ya Usafiri wa Anga ya mkoa wa Somaliland siku ya Jumanne (tarehe 18 Juni) iliikataza ndege...
Polisi nchini Tanzania waliwakamata makamu wanne wa chama kikuu cha upinzani cha Demokrasia na Ma...
Watu wenye silaha kwenye Kaunti ya Wajir walimuua polisi mmoja wa akiba wa Kenya siku ya Jumanne ...
Japan inaipa Tanzania dola milioni 49 (shilingi bilioni 80.4) kama msaada na mkopo kwa ajili ya k...
Inspekta Jenerali wa Polisi David Kimaiyo yeye pekee yake amewateua na kuwapangia kazi maafisa wa...
Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) siku ya Jumanne ilimkubalia Makamu wa Rais wa Kenya Willia...
Polisi waliwakamata mamia ya watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa al-Shabaab katika wilaya za Hod...
Kongamano la siku tatu juu ya elimu lilifunguliwa mjini Mogadishu siku ya Jumanne (tarehe 18 Juni...
Wanajeshi wa serikali ya Somalia wakisaidiwa na wanajeshi wa Misheni wa Umoja wa Mataifa (AMISOM)...
Waziri wa Mambo ya Ndani na Uratibu wa Serikali ya Kitaifa, Joseph Ole Lenku, siku ya Jumatatu (t...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji
Maoni ya msomaji
Kwa bahati mbaya, Waafrika wa Kenya, wanataka fedha na utalii (bila ya kufanya kazi kwa bidii). Watalii wa nchi za Ghuba wanajali kuhusu usalama na usafi.