Tanzania yatumia kifaa cha mtandaoni kwa ajili ya wawekezaji

Agosti 17, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Tanzania imeanzisha kifaa cha mtandaoni ili kuwasaidia wawekezaji na wajasiriamali kupata kwa urahisi habari za kisasa kuhusu taratibu zinazohusiana na uwekezaji, gazeti la Tanzania la Daily News liliripoti hapo Ijumaa (tarehe 17 Agosti).

Kituo cha uwekezaji Tanzania (TIC) kwa sasa kinafuata mfumo huo unaojulikana kama "Taratibu za mtandaoni" (e-Regulations), kilichotengenezwa na Mkutano wa Umoja wa Mataifa juu ya Biashara na Maendeleo (UNCTAD).

"Wakati taratibu na hatua hizi zinazohusika zitakapojulikana na watu ungetarajia watu zaidi kuanza biashara na ongezeko la uwajibikaji katika kulipa kodi," alisema Kjartan Sorensen, meneja uwezeshaji biashara wa UNCTAD mwenye dhamana ya Taratibu za mtandaoni barani Afrika.

Kwa mujibu wa UNCTAD, taratibu za mtandaoni zinaweza kuchangia sana uwazi na ufanisi katika huduma za umma, kuimarisha uendeshaji na kupunguza gharama.

Ingawa mfumo huu uko katika benki ya data mtandaoni, wawekezaji na wajasiriamali wanaweza kupata habari za lazima za biashara, ikiwa ni pamoja na jinsi ya kuandikisha kampuni, kulipa kodi na kupata viza au cheti cha vichocheo katika TIC.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 1)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo