Agosti 17, 2012
Mahakama Kuu ya Kenya ilihukumu siku ya Alhamisi (tarehe 16 Agosti) kwamba Wairani wawili wanaotuhumiwa kwa ugaidi ambao waliachiwa kwa dhamana mwezi uliopita watabakia chini ya uangalizi wa polisi hadi kesi zao zitakaposhughulikiwa, Star ya Kenya iliripoti.
Watuhumiwa hao wawili, Ahmed Mohamud na Sayed Mausud, walishitakiwa kwa kumiliki kilogramu 15 za mabomu yenye nguvu kubwa ya RDX katika maandalizi ya kufanya mashambulizi kwa Wakenya. Mwanasheria Lydia Achode alisema kukamatwa kulikuja baada ya taarifa za kuaminika zilizopendekeza kwamba kilogramu 100 za RDX zimesafirishwa kutoka Iran hadi Kenya, kilo 85 kati ya hizo hazikurejeshwa.
Mahakama hiyo Kuu ilibatilisha uamuzi wa mahakama ya chini wa kuwaachia watuhumiwa hao kwa dhamana ya shilingi milioni 2 (Dola za Kimarekeni 23,800) kwa kila mmoja mwezi uliopita.
Achode alisema Kenya haijasainiana na Iran mkataba wa watuhumiwa kuhukumiwa katika nchi waliyokosa (Kenya) na haieleweki kama watuhumiwa watarejea Kenya kwa ajili ya utekelezaji wao wa kurudi nchini kwao.
Alifuta madai yao kwamba walitakiwa kuachiwa huru kupata matibabu na kuona matunzo yaliyotolewa katika gereza yanatosheleza.
Kama watakutwa na makosa, Mohamud na Mausud watakuwa na uwezekano wa kufungwa gerezani.
Makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto, alisema kazi za Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia ...
Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia siku ya Alhamisi (tarehe 16 Mei) alipokea vyeti vya utambul...
Kwa uchache watu wanne waliuawa na watatu kujeruhiwa siku ya Alhamisi (tarehe 16 Mei) baada ya wa...
Kenya na Tanzania zilifanya operesheni ya pamoja ya ulinzi wa mpaka siku ya Alhamisi (tarehe 16 M...
Mwanachama wa kundi la wanamgambo wanaoiunga mkono serikali ya Somalia la Ahlu Sunna wal Jamaa, A...
Wanawake watatu waliuawa usiku wa Alhamisi (tarehe 16 Mei) katika eneo la Malkamau kwenye Kaunti ...
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon. siku ya Alhamisi (tarehe 16 Mei) alimteua waziri wa...
Tanzania na Canada zimesaini mkataba wa ushirikiano yanayokusudiwa kuimarisha na kuunda mazingira...
Jeshi la Taifa la Somalia liliwauwa wanamgambo 13 wa al-Shabaab siku ya Jumanne (tarehe 14 Mei), ...
Muda wa mwisho kwa wakaazi wa Mandera kusalimisha silaha zao haramu umeongezwa hadi Ijumaa (tareh...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji