Agosti 17, 2012
AMISOM itaendelea kutoa kipaumbele katika kuwalinda raia wa Somalia katika mgogoro wa kijeshi unaoendelea nchini Somalia, Mwakilishi Maalumu wa Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia Boubacar Diarra alisema Alhamisi (tarehe 16 Agosti).
"AMISOM inachukua jukumu lake kwa usalama wa wananchi wa Somalia kwa uzito mkubwa na inaelewa kikamilifu wajibu wake wa kuendesha operesheni bila ya kusababisha hatari kwa wananchi wenyeji," Diarra alisema.
Alisema wananchi wa Somalia ni muhimu katika mafanikio ya misheni ya AMISOM. Alionyesha "masikitiko makubwa" kuhusiana na ripoti za majeruhi wa kiraia huko Kismayo, akiongeza kwamba ripoti hizo zitachunguzwa.
Ripoti zilionya kwamba meli za kivita zilizotia nanga katika pwani ya Kismayo zilirushiana risasi na wapiganaji wa al-Shabaab katika mji Jumamosi, zikiwaua watu watatu na kujeruhi wanne.
"Tunaviomba vikosi vingine vya kijeshi kuweka vizuizi vinavyostahili katika maeneo yenye idadi kubwa ya raia," alisema.
Watumishi wa AMISOM wamekuwa wakifundishwa katika dhana ya sheria za binadamu za kimataifa na wana sera za kuwalinda wananchi, ikiwa ni pamoja na kutokuwa na kanda zisizo na moto katika maeneo yenye wananchi wengi, alisema, akiongeza kwamba jitihada za AMISOM kupunguza madhara kwa wananchi zimetambuliwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na mawakala wa kimataifa.
Ujumbe kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya Pembe ya Afrika (IGAD) uliwatembelea maafisa mjini Mogadish...
Mshukiwa wa ugaidi na mke wake walipigwa risasi na kufa na maafisa sita wa polisi walijeruhiwa wa...
Watu watano walikamatwa siku ya Jumanne mjini Dar es Salaam wakiwa na vifaa vya kulipua katika mi...
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta aliwataka wabunge kuweka kando madai yao ya kuongezwa mishahara kwa ...
Majeshi ya serikali ya Somalia waliwaua wanamgambo tisa wa al-Shabaab wakati wa mapambanao hapo J...
Mtu asiyejulikana alimpiga kwa risasi na kumuua ofisa wa kitengo cha usalama cha kijeshi huko kas...
Muungano wa Jubilee tawala cha Kenya kilichukua uongozi wa kamati mbili muhimu za bunge Ijumaa (t...
Chama cha Wafanyabiashara na Asasi ya Chakula na Kilimo ya Umoja wa Mataifa vinatoa mafunzo kwa w...
Balozi wa Umoja wa nchi za Ulaya nchini Tanzania Filiberto Ceriani Sebregondi aliwahamiza waandis...
Makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto, alisema kazi za Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia ...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji
Maoni ya msomaji
Inafurahisha kuona kuwa dunia inajali kuhusu masuala ya Somalia, kwa sababu itawasaidia watu wa Somalia. Lakini haitakuwa na faida yoyote ikiwa Wasomali hawakushirikiana wao kwa wao ili kutatua matatizo yao. Ikiwa hawakuungana na kuwa na hamira ya kutatua mizozo yao ya ndani, jaribio lolote la kutatua suala hili kutoka nje litashindwa.
Ninawaombea AMISOM WAFANYE KAZI KWA UMOJA ili kuleta kanuni katika Pembe ya Afrika. Watu wa SOMALIA LAZIMA WAKUBALI msaada wa nje uliopo ILI KULETA UTULIVU katika nchi yao.