Red_arrow

Ungependa kuifanya Kiswahili kuwa lugha ya chaguo lako, katika tovuti hii? |

Kenya kupigania kuandaa Michezo ya Olimpiki 2024

Agosti 10, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Kenya inadhamiria kuwasilisha ombi la kuwa nchi ya kwanza barani Afrika kuwa mwenyeji wa Michezo ya Olimpiki 2024, liliripoti gazeti la Financial Times hapo Ijumaa (tarehe 10 Agosti).

"Kenya ilikuwa na imani hiyo tangu mwaka 1968 kufikiria kuandaa michezo ya Olimpiki," alisema Waziri Mkuu Raila Odinga akiwa jijini London. "Hiyo ni imani tunayohitaji kuwa nayo tena. Tunahitaji kuirudisha imani hiyo na tunaweza kufanya hivyo. Ni muhimu kuangalia nyuma kule tulikotoka na wapi tunataka kwenda, kwa sababu tumekuwa tukijikokota kwa muda mrefu mno," alisema.

Odinga alisema miundombinu na biashara ya Kenya itavuna "faida kubwa sana" kutokana na uwekezaji ambao ni lazima katika kuwa mwenyeji wa Olimpiki.

Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki imeelezea hamu yake ya kupokea maombi kutoka kwa nchi za Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara, kwa mujibu wa gazeti la Financial Times. Afrika ya Kusini, Qatar, Marekani, Morocco, Misri na Argentina zimetajwa kama wagombea katika kutayarisha Michezo ya 2024.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo