Baraza la Usalama la Umoja Mataifa lawaonya wanaozuia mchakato wa amani

Agosti 10, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Baraza la usalama la Umoja wa mataifa katika taarifa yake ya Alhamisi (tarehe 9 Agosti) iliwalaani wale wote wanaojaribu kuzuia mchakato wa amani wa Somalia.

"Wanachama wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wanalaani vikali majaribio yanayoendelea, yakiwemo kutoka kwa al-Shabaab, ya kuzuia mchakato wa mpito," taarifa ilisema. "Wanazungumzia hili kuhusiana na dhamira ya baraza la usalama na kuchukua hatua dhidi ya wote, wa ndani na wa nje watakaojihusisha na vitendo vinavyokusudia kuzuia mchakato wa amani na maelewano."

Baraza la Usalama pia lilitoa wito kwa wabunge kuchaguliwa haraka katika njia ya uwazi.

Mwakilishi Maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia, Augustine Mahiga, ameripoti matukio ya utishiaji na rushwa katika mchakato wa uteuzi. Wiki hii, pia aliwataka viongozi wa Somalia kushikamana na tarehe 20 Agosti kuwa ndio tarehe ya mwisho kukamilisha mpito na kuanza kwa serikali ya kudumu.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, serikali za majimbo ya shirikisho ziundwe vipi nchini Somalia kufuatia utata wa Jubbaland?

Angalia matokeo