Polisi ya Kenya yawaorodhesha wazee kusaidia katika uchaguzi mkuu

Agosti 10, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Polisi ya Kenya na Kamisheni ya Umoja wa Kitaifa na Maingiliano (NCIC) wameomba msaada wa wazee wa makabila kuepuka ghasia katika uchaguzi wa mwaka 2013, liliripoti gazeti la nchi hiyo la Daily Nation hapo Alhamis (tarehe 9 Agosti).

"Mazingira ya kisiasa kuelekea uchaguzi mkuu wa 2013 ni tofauti na yale ya mwaka 2007. Sheria mpya imetupa mamlaka mengi na kila mtu atalazimika kukabiliana na sheria," alisema makamo wa msemaji wa polisi Charles Owino. "Hatutaki kusubiri hadi hatari zitokee na ndio maana tunajumuisha wazee wa jamii kama chanzo cha kutatua mizozo," alisema.

Juhudi za polisi zitaelekezwa zaidi katika majimbo 29 yaliyoainishwa kuwa ndiyo yanaweza kuwa "vyanzo moto" vya mizozo.

"Wakenya wa leo wana imani kubwa na polisi na tunaweza kulishughulikia hilo," Owino alisema. "Ukweli kwamba mkuu mpya wa polisi atakuwa huru kutojihusisha na mafungamano yoyote ya kisiasa hilo litafaa kwa kuongeza imani zaidi."

Kamati elekezi ya taifa ikiwa na wawakilishi kutoka polisi, Wizara ya Habari, Tume ya Mawasiliano ya Kenya, Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka pamoja na NCIC pia zitasimamia vyombo vya habari na kuhamasisha kuimarisha umoja wa kitaifa.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 2)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo