Farmajo arudi Mogadishu kuanza kampeni za uraisi, maandamano yashambuliwa na majambazi

Agosti 10, 2012

  • 1 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Waziri Mkuu wa zamani wa Somalia, Mohamed Abdullahi Farmajo, alirejea Mogadishu hapo Alhamis (tarehe 9 Agosti), mwaka mmoja baada ya kujiuzulu wadhifa wake, kuzindua kampeni ya uraisi.

  • Wafuasi wa Waziri Mkuu wa zamani wa Somalia, Mohamed Abdullahi Farmajo, wakikusanyika katika mitaa ya Mogadishu wakati wa maandamano ya kampeni za uchaguzi kumuunga mkono kwa kugombea uraisi. [Adnan Hussein/Sabahi]

    Wafuasi wa Waziri Mkuu wa zamani wa Somalia, Mohamed Abdullahi Farmajo, wakikusanyika katika mitaa ya Mogadishu wakati wa maandamano ya kampeni za uchaguzi kumuunga mkono kwa kugombea uraisi. [Adnan Hussein/Sabahi]

Wakaazi wa Mogadishu walikusanyika kwa kiwango kikubwa karibu na uwanja wa ndege wa Mogadishu na barabara ya Maka al-Mukarama kumkaribisha mgombea huyo wa uraisi.

Hata hivyo, majambazi wasiojulikana waliwashambulia waandamanaji kwa risasi, wakauwa watu wawili na kuwajeruhi wengine kadhaa katika eneo la Sayid Mohamed Abdullahi Hassan, karibu na jengo la bunge.

Farmajo amedai kufanyike uchunguzi kamili wa tukio hilo.

Mfuasi wa Farmajo aitwaye Siham Yunis, ambaye alikuwapo kwenye tukio, aliiambia Sabahi kwamba maandamano yalianza uwanja wa ndege na yalipokuwa yakikaribia mzunguko wa Sayid, watu wenye bunduki walirusha risasi kuelekea upande wao, wakaua na kuwajeruhi wafuasi kadhaa. Alisema baadhi ya wafuasi hao walifariki dunia wakati wakipelekwa hospitali.

Kufuatia mkasa huo, maafisa wa jeshi na usalama wa taifa walilifunga eneo hilo kwa lengo la kudhibiti hali.

Hakuna kundi ambalo limedai kuhusika na kuwalenga waandamanaji, na hakuna yeyote hadi sasa aliyekwishakamatwa kwa kuhusishwa na tukio hilo. Baraza la Mawaziri la Somalia limeviamrisha vikosi vya usalama kuchunguza kadhia hiyo na kumaliza hujuma kama hizo zinazofanywa na makundi yenye silaha yanayotaka kuuzorotesha usalama kwenye mji mkuu.

Farmajo alikuwa waziri mkuu wa Somalia kutoka Oktoba 2010 hadi Juni 2011 alipojiuzulu kama sehemu ya Makubaliano ya Kampala yaliyoongeza muda wa serikali ya mpito hadi Agosti 2012.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 4)

Dislike_icon(1)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • samiir
    August 13, 2012 @ 09:20:09AM

    Habari hii sio sahihi kwa sababu wale waliowapiga watu risasi walikuwa majeshi ya Sheikh Sharif.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo