Agosti 07, 2012
Vikosi vya majeshi ya Somalia na Ethiopia viliwaua zaidi ya wanamgambo 30 wa al-Shabaab baada ya wanamgambo hao kukishambulia kituo chao huko Hudur hapo Jumatatu (tarehe 6 Agosti), iliripoti redio inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa ya Bar-Kulan.
Al-Shabaab walidai kwamba waliwaua zaidi ya wanajeshi 60 wa Ethiopia wakiwemo makamanda wanne wa ngazi za juu, kwa mujibu wa taarifa ya kundi hilo kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter.
Idadi kamili ya walioathirika kutokana na tukio hilo haiwezi kuthibitishwa na vyanzo huru.
Mapigano hayo yalichukuwa masaa saba, alisema Mkuu wa Wilaya Mohamed Moalim Ahmed, yakiwajeruhi wanamgambo wengine 12. Hakusema chochote kuhusiana na hasara kwa upande wa vikosi vya washirika katika makabiliano hayo.
Haya ni mashambulizi ya pili dhidi ya vikosi vya Somalia wilayani Hudur tangu mwanzo wa Ramadhani. Vikosi vya washirika viliukamata mji huo kutoka mikononi mwa al-Shabaab mwezi Machi.
Polisi nchini Tanzania walimkamata mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msingwa, na wafanyabiashara 60 k...
Mahakama moja ya Bosaso iliwatia hatiani na kuwapiga faini Wairani 78 siku ya Jumapili (tarehe 19...
Polisi nchini Tanzania waliwakamata watuhumiwa 15 kuhusiana na kulichoma Kanisa la Bethania kweny...
Mkuu wa Polisi wa Kenya, David Kimaiyo, ameondoa nafasi za afisa polisi wa jimbo, afisa wa upelel...
Watu wenye silaha waliwaua watu wawili na kuwajeruhi wengine wanne katika mashambulizi tofauti kw...
Mkutano wa kuzungumzia uwezekano wa uchimbaji mafuta na gesi, uwekezaji, usalama na miundombinu n...
Wizara ya Masuala ya Wanawake na Familia ya Puntland ilianza mafunzo ya siku nane hapo Juampili (...
Zaidi ya Wasomali milioni 1 hawatakuwa na "usalama wa chakula" hadi mwezi wa Septemba, Mtandao wa...
Ujumbe kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya Pembe ya Afrika (IGAD) uliwatembelea maafisa mjini Mogadish...
Mshukiwa wa ugaidi na mke wake walipigwa risasi na kufa na maafisa sita wa polisi walijeruhiwa wa...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji