Wadhamini wa Mpango Mkuu wa Somalia wazungumzia kumalizika kwa utawala wa mpito

Agosti 07, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Wadhamini wa Mpango Mkuu ya Somalia waliokutana jijini Nairobi walitoa rasimu ya tamko hapo Jumatatu (tarehe 6 Agosti ) kuzungumzia hatua zilizobakia kukamilisha kipindi cha utawala wa mpito.

Tamko hilo lililotolewa na Ofisi ya Siasa ya Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Somalia (UNPOS), ilitatua mivutano inayoendelea kati ya wakuu wa makabila kutoka kabila la Dhulbahante kaskazini ya Somalia kuhusiana na uchaguzi wa kundi la wabunge, na kurudia msimamo wake kwamba uchaguzi wa wabunge, rais na spika utafuata Makubaliano ya Garowe .

Washiriki pia walitaka kuwepo kwa usalama wa wajumbe wa Kamati ya Ufundi, ambao wamepewa jukumu la kuhakikisha uadilifu na uwazi katika utaratibu wa uchaguzi. UNPOS itachukua hatua za haraka kuongeza ulinzi kwa wajumbe wa kamati hiyo, ilisema taarifa hiyo.

Wajumbe waliosaini tamko hilo walirejelea msimamo wao kwamba rushwa na vitisho havitavumiliwa wakati wa utaratibu wa uteuzi.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 4)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo