Julai 30, 2012
Mamlaka ya Barabara Kuu ya Kenya (KENHA) itafunga barabara kadhaa za Nairobi wakati wa ujenzi wa barabara mpya ya upande wa kusini wa mji huo, liliripoti gazeti la Kenya la Daily Nation siku ya Jumapili (tarehe 29 Julai).
KENHA itazifunga kabisa barabara za Community, Kibera na Nong, au kupunguza matumizi yake, kwa miezi sita ijayo, kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa KEHNA, Mishack Kidenda. Alisema waendesha vyombo vya maringi mawili watumie njia nyingine zilizowekwa kufikia barabara ya Lang'ata.
Barabara hizo zitafungwa kupisha ujenzi wa njia ya kusini mwa Nairobi, inayokusudiwa kupunguza msongomano katika mji mkuu huo.
Waziri wa Usafiri wa Haraka wa Nairobi, Jamlek Irungu Kamau alisema Nairobi imo kwenye mfululizo wa uimarishaji wa miundombinu yake. Miradi hiyo inajumuisha matengenezo ya barabara na uwekaji wa taa za mitaani katika baadhi ya masoko.
Benki ya Dunia imeikopesha Kenya dola milioni 600 (shilingi bilioni 50.5) kuimarisha huduma. Kiasi ya nusu ya fedha hizo zimetengwa kwa ajili ya Mradi wa Kuimarisha Usafiri wa Haraka wa Nairobi unaokusudiwa kuimarisha miundombinu katika mkoa huo wa mji mkuu.
Wizara ya Usafiri wa Anga ya mkoa wa Somaliland siku ya Jumanne (tarehe 18 Juni) iliikataza ndege...
Polisi nchini Tanzania waliwakamata makamu wanne wa chama kikuu cha upinzani cha Demokrasia na Ma...
Watu wenye silaha kwenye Kaunti ya Wajir walimuua polisi mmoja wa akiba wa Kenya siku ya Jumanne ...
Japan inaipa Tanzania dola milioni 49 (shilingi bilioni 80.4) kama msaada na mkopo kwa ajili ya k...
Inspekta Jenerali wa Polisi David Kimaiyo yeye pekee yake amewateua na kuwapangia kazi maafisa wa...
Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) siku ya Jumanne ilimkubalia Makamu wa Rais wa Kenya Willia...
Polisi waliwakamata mamia ya watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa al-Shabaab katika wilaya za Hod...
Kongamano la siku tatu juu ya elimu lilifunguliwa mjini Mogadishu siku ya Jumanne (tarehe 18 Juni...
Wanajeshi wa serikali ya Somalia wakisaidiwa na wanajeshi wa Misheni wa Umoja wa Mataifa (AMISOM)...
Waziri wa Mambo ya Ndani na Uratibu wa Serikali ya Kitaifa, Joseph Ole Lenku, siku ya Jumatatu (t...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji
Maoni ya msomaji
Hii ndio njia ya kuelekea Dira 2030. Wakenya wote tuunge mkono maendeleo haya bila ya kujali upande wao siasa/vyama. Hongera serikali.
Ninathamini barabara za kando lakini nachukia usumbufu. Kazi lazima ifanywe kwa hivyo ujenzi wa barabara uanze.