Julai 30, 2012
Mataifa sita ya Afrika Mashariki yako hatarini kuingia kwenye ukosefu mkubwa wa chakula huku watu wapatao milioni 16 wakiathirika katika kiwango kikubwa, kwa mujibu wa ripoti ya mwezi Julai ya Mtandao wa Kutoa Onyo la Ukame (FEWSN).
Onyo hilo la FEWSN linahusu nchi za Kenya, Djibouti, Ethiopia, Sudan, Sudan ya Kusini na Uganda, kunakosababishwa na upungufu wa mvua, migogoro, bei kubwa za chakula na baadhi ya wakati kutokuwa na uwezo wa kupata misaada ya kibinaadamu. Mtandao huo wa FEWSN ulioanzishwa na Shirika la Misaada ya Kimataifa la Marekani (USAID, linashirikiana na washirika wa kimataifa na wa eneo hilo kutoa taarifa za mapema za kuonya juu ya masuala ya usalama wa chakula.
Mvua katika maeneo ya kusini mashariki ya Kenya kutoka Machi hadi Mei zilikuwa za muda mfupi mwaka huu na maeneo ya kusini ya mkoa huo yanaweza kukifikia kiwango cha upungufu wa chakula, ilisema ripoti hiyo.
Msaada wa kibinaadamu wa chakula umefanya bei za chakula kutulia, pale hali ilipofikia kiwango cha njaa katika mwaka 2011. Hata baada ya kuimarishwa, bado zaidi ya asilimia 15 ya watu wanakabiliwa na kiwango kibaya cha utapiamlo katika maeneo kadhaa nchini humo.
Maeneo yanayotegemea kilimo kusini mwa Somalia, ikiwemo mikoa Bay, sehemu za Juba, Shabelle, Bakol na Gedo pia ilipata mvua za kiwango cha chini na zilizocholewa katika msimu wa mwaka huu wa mvua kuanzia Aprili hadi Juni, liliripoti shirika hilo.
Makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto, alisema kazi za Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia ...
Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia siku ya Alhamisi (tarehe 16 Mei) alipokea vyeti vya utambul...
Kwa uchache watu wanne waliuawa na watatu kujeruhiwa siku ya Alhamisi (tarehe 16 Mei) baada ya wa...
Kenya na Tanzania zilifanya operesheni ya pamoja ya ulinzi wa mpaka siku ya Alhamisi (tarehe 16 M...
Mwanachama wa kundi la wanamgambo wanaoiunga mkono serikali ya Somalia la Ahlu Sunna wal Jamaa, A...
Wanawake watatu waliuawa usiku wa Alhamisi (tarehe 16 Mei) katika eneo la Malkamau kwenye Kaunti ...
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon. siku ya Alhamisi (tarehe 16 Mei) alimteua waziri wa...
Tanzania na Canada zimesaini mkataba wa ushirikiano yanayokusudiwa kuimarisha na kuunda mazingira...
Jeshi la Taifa la Somalia liliwauwa wanamgambo 13 wa al-Shabaab siku ya Jumanne (tarehe 14 Mei), ...
Muda wa mwisho kwa wakaazi wa Mandera kusalimisha silaha zao haramu umeongezwa hadi Ijumaa (tareh...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji