Julai 30, 2012
Chama cha Msalaba Mwekundu cha Tanzania kitazindua programu ya kuwafundisha wafanyakazi wake wa kujitolea kuhusiana na matayarisho ya majanga, uokozi na huduma ya mwanzo, alisema Katibu Mkuu wa chama hicho alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
"Vile vile tunapanga kuliimarisha tawi letu la Zanzibar kuwa na uwezo wa kukabiliana na majanga kwa ufanisi wakati wowote yanapotokea," alisema Kimbisa, liliripoti gazeti la Tanzania la Daily News siku ya Jumatatu (tarehe 30 Julai).
Programu hiyo itafadhiliwa kwa shilingi milioni 10 (dola 6,300) zilizotolewa na mfanyabiashara Samantar Abdinur Iusuf, kwa kutambua mchango wa Chama cha Msalaba Mwekundu katika operesheni ya kuwaokoa wahanga wa ajali ya meli ya MV Star Gates iliyotokea kati ya Tanzania Bara na Zanzibar katikati ya mwezi huu.
Wafanyakazi 65 wa kujitolea na watatu wa kudumu waligawa mablanketi 200, mifuko 200 ya kuhifadhia maiti, glovu 200 na vifaa 200 vya kuvaa usoni wakati wa jitihada za uokozi.
Kimbisa alisema sehemu ya fedha hizo itatumika kununua vifaa vya uokozi na zilizobakia zitakwenda kwa wahanga wa ajali hiyo.
Wizara ya Usafiri wa Anga ya mkoa wa Somaliland siku ya Jumanne (tarehe 18 Juni) iliikataza ndege...
Polisi nchini Tanzania waliwakamata makamu wanne wa chama kikuu cha upinzani cha Demokrasia na Ma...
Watu wenye silaha kwenye Kaunti ya Wajir walimuua polisi mmoja wa akiba wa Kenya siku ya Jumanne ...
Japan inaipa Tanzania dola milioni 49 (shilingi bilioni 80.4) kama msaada na mkopo kwa ajili ya k...
Inspekta Jenerali wa Polisi David Kimaiyo yeye pekee yake amewateua na kuwapangia kazi maafisa wa...
Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) siku ya Jumanne ilimkubalia Makamu wa Rais wa Kenya Willia...
Polisi waliwakamata mamia ya watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa al-Shabaab katika wilaya za Hod...
Kongamano la siku tatu juu ya elimu lilifunguliwa mjini Mogadishu siku ya Jumanne (tarehe 18 Juni...
Wanajeshi wa serikali ya Somalia wakisaidiwa na wanajeshi wa Misheni wa Umoja wa Mataifa (AMISOM)...
Waziri wa Mambo ya Ndani na Uratibu wa Serikali ya Kitaifa, Joseph Ole Lenku, siku ya Jumatatu (t...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji
Maoni ya msomaji
Makala hii ni nzuri ila ni vyema sisi wanachama wa Redcross kuwe na utaratibu wa kukutana walau hata kwa mwaka mara tatu kwa lengo ya kukumbushana majukumu ya kazi na kama kuna tarifa mpya na mbinu nyingine za kisasa za huduma ya kwanza au uokoaji. Asante