Umoja wa nchi za Ulaya wasema Somalia lazima isivuke muda wa mwisho wa kumalizika kwa kipindi cha mpito

Julai 24, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Viongozi na wadau wa Somalia wanapaswa kuheshimu muda wa mwisho uliowekwa kwa serikali ya kipindi cha mpito hapo tarehe 20 Agosti na wafanye kazi kwa ajili ya maslahi ya watu wa Somalia, limesema Baraza la Umoja wa Ulaya hapo siku ya Jumatatu (tarehe 23 Julai).

Baraza hilo lilipongeza makubaliano juu ya katiba ambayo wadhamini wa Mpango wa Amani wa Somalia jijini Nairobi mwezi uliopita, lakini likaeleza wasiwasi wake kwamba "kuendelea kusogezwa mbele na kukosekana kufikiwa kwa muda wa mwisho kunahatarisha uwazi na uhalali wa utaratibu wa kisiasa ulioanzishwa na Makubaliano ya Garowe ".

"Kuongezwa kwa muda wa taasisi za serikali ya mpito hakutakubalika na juhudi za kukwaza mageuzi halali nchini Somalia zitakabiliwa na hatua kali zinazostahiki," ilisema taarifa ya baraza hilo.

Umoja wa Ulaya "unautaka uongozi wa Somalia kufanya kazi kwa uwazi na kutoa taarifa kwa umma katika kipindi hiki kilichobakia," lilisema baraza hilo, likisisitiza umuhimu wa kutekeleza ahadi yake ya kuwa na asilimia 30 ya wanawake kwenye serikali ya shirikisho.

Baraza hilo liliwatolea wito wazee wa makabila nchini Somalia kukamilisha haraka uteuzi wa wajumbe wa Bunge la Katiba ili rasimu ya katiba iweze kuidhinishwa na kupigiwa kura ya maoni.

Mkutano wa Bunge la Katiba umeahirishwa mara kadhaalakini sasa umepangwa kufunguliwa mjini Mogadishu hapo siku ya Jumatano.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 2)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo