NATO yapata mafanikio katika kupambana na uharamia

Julai 22, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Vitisho vya uharamia katika bahari ya Somalia vinapungua, kamanda wa kupambana na ugaidi wa Jumuiya ya Makubaliano ya Atlantiki ya Kaskazini (NATO) Commodore Ben Bekkering alisema hapo Jumamosi (tarehe 21 Julai).

"Tunapata mafanikio zaidi katika kupunguza vitisho vya uharamia wa Somalia kutokana na doria yetu mfululizo, lakini jumuiya ya kimataifa lazima iendelee kubadilishana mawazo ili kumaliza tatizo hili moja kwa moja," Bekkering alisema, kwa mujibu wa gazeti la Times la Omani.

Ofisi ya Kimataifa ya Bahari ilirikodi matukio 69 ya ugaidi yanayoyawahusu Wasomalia baina ya mwezi Januari na Julai mwaka huu, na kufanya anguko la asilimia 32 ikilinganishwa na mwaka 2011, kwa vile vikosi vya jeshi la majini vya kimataifa viliongeza juhudi zake.

Bekkering alisema uharamia wa Somalia unaendelea kusababisha upotevu wa mamilioni ya dola katika biashara ya kimataifa kila mwaka. "Ni muhimu tufanye kazi pamoja ili kuuzuia," alisema.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, katiba ya Kenya inapaswa kurekebishwa ili kulipa baraza jipya la Seneti madaraka zaidi?

Angalia matokeo