Wanaolimpiki wa Somalia wawasili London

Julai 22, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Zamzam Mahmuud Farah na Mohamed Hassan Mohamed, wawakllishi wa Somalia katika Olimpiki , walipokewa na mashabiki mjini London siku ya Ijumaa (tarehe 20 Julai), Redio RBC ya Somalia iliripoti.

Wanachama wa Jumuiya ya Wasomali waliopo London walikutana na wanariadha katika kijiji cha Olympiki wakipeperusha bendera ya Somali na kuimba Wimbo wa Taifa.

"Leo nimefurahi sana kwa sababu sijawahi kufikiria ningekutana na wanariadha wa Somalia wakiwakilisha nchi yetu, lakini imetokea leo," Hafsa Farah Msomali anayeishi Uingereza mwenye umri wa miaka 19 alisema wakati wa sherehe ya ukaribisho.

Farah alisema michezo inaweza kusaidia kukabiliana na matatizo ya kisiasa nchini Somalia. "Michezo inaweza kuwaunganisha watu," alisema, kwa mujibu wa gazeti la Somalia Report. "Inaweza kuwa na nafasi kubwa katika kuunganisha jamii zinazopinzana."

Farah atakimbia katika mashindano ya mbio za meta 400, na Mohamed katika mashindano ya mbio za meta 1,500.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 3)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo