Ahlu Sunna wal Jamaa wapongeza kurudi kwa Shirika la Chakula Mataban

Julai 13, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Kundi la wanamgambo wanaoiunga mkono serikali ya Somalia, Ahlu Sunna wal Jamaa (ASWJ) limelipongeza Shirika la Chakula Duniani (WFP) kwa kurudisha operesheni za misaada katika wilaya ya Mataban mkoani Hiran, iliripoti Redio Bar-Kulan inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa hapo Alhamis (tarehe 12 Julai).

Kamishna wa kundi la ASWJ katika wilaya hiyo, Abdirahman Abdi Mohamed, alisema kurudi kwa shirika la WFP ni hatua muhimu katika kuishughulikia hali mbaya ya kibinaadamu katika wilaya hiyo,ambako kunaishi wakimbizi wa ndani wa Kisomali wapatao 8,000.

Shirika la WFP liliondoka Mataban kufuatia mauaji ya wafanyakazi wake wawili hapo mwezi Februari.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 2)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo