Polisi wa Kenya wajeruhiwa karibu na Somalia

Julai 13, 2012

  • 1 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Askari wawili wa Kenya walipigwa risasi na kujeruhiwa vibaya katika mashambulizi yanayotajwa kufanywa na wapiganaji wa al-Shabaab hapo Alhamis (tarehe 12 Julai), kiliripoti kituo cha redio cha Capital FM cha Kenya.

Maafisa hao wa polisi walikuwa wakirudi kutoka Garissa kupitia eneo la Arabia, karibu na mpaka wa Somalia, pale watu wenye silaha walipoanza kuwarushia risasi.

"Watu hao wenye silaha walikuwa kwenye makundi na walituchawanyia risasi nasi tukawajibu," alisema naibu mkuu wa polisi, John Mbaluka.

Wiki mbili zilizopita, watu wenye silaha waliwaua watu 17 na kuwajeruhi wengine kadhaa katika mashambulizi yaliyolenga makanisa mawili mjini Garissa.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 5)

Dislike_icon(4)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • dahir
    July 14, 2012 @ 03:48:16PM

    Ni tendo baya kuua watu wasio na hatia ambao ni wapenda amani.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo