AMISOM waurudisha msaada wa chakula uliokuwa umeibiwa na al-Shabaab

Julai 13, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Wanajeshi wa kikosi cha Umoja wa Afrika mjini Mogadishu wamefanikiwa kuyarudisha zaidi ya magunia 500 ya chakula kilichoibiwa kutoka kwenye kambi ya al-Shabaab iliyotekwa katika eneo la Laanta Buuro, ilisema taarifa ya AMISOM hapo Alhamis (tarehe 12 Julai).

Chakula hicho kilikuwa kimekusudiwa kwa msaada wa kibinaadamu, lakini al-Shabaab ilikuwa inakitumia kulisha wapiganaji wake katika kambi hiyo, umbali wa kilomita 40 magharibi ya Mogadishu. Chakula hicho sasa kimerudishwa kwa watu wa eneo hilo.

Wapiganaji 11 wa al-Shabaab waliuawa na wanne wakakamatwa mateka baada ya AMISOM kuichukua kambi hiyo hapo Jumatano, ilisema taarifa hiyo. AMISOM ilitangaza kwamba pia ilikamata rundo la silaha, zikiwemo bunduki na vifaa vya kutengenezea mabomu.

Kamanda wa AMISOM, Luteni Jenerali Andrew Gutti, alisema hivi karibuni mashirika ya misaada yataweza kuingia kwenye maeneo ambayo hadi karibuni yalizuia na al-Shabaab. "Tunatimiza wajibu wetu kusaidia utaratibu wa amani wa Somalia na kuandaa mazingira mazuri kwa ajili ya ufikishaji wa misaada ya kibinaadamu inayohitajika sana," alisema.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 7)

Dislike_icon(1)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo