Wafanyakazi 3 wa misaada watekwa nyara Somalia

Julai 12, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Wafanyakaazi wawili wa misaada wa Kenya na daktari wa Kisomali walitekwa nyara huko Somalia siku ya Jumatano (tarehe 11 Julai), polisi walisema.

Utekaji nyara huo ulitokea karibu na mji wa Galkayo, unaogawa mpaka baina ya jimbo la kaskazini lenye serikali ya ndani na mkoa wa Galmudug.

"Wakenya wawili na daktari mmoja wa Kisomali walitekwa nyara na taarifa za mwanzo zinaashiria kuwa wateka nara walikuwa maharamia, lakini bado tunachunguza juu ya tukio hili," alisema Adan Warsame, afisa ndani ya polisi ya Galkayo, aliiambia AFP.

Mohammed Ise Hassan, afisa mwingine wa polisi, alisema dereva na walinzi wawili walijeruhiwa katika utekaji nyara huo.

Watu hao watatu waliotekwa nyara ni waajiriwa wa shirika lisilo la kiserikali la Sweden International Aid Services. Shirika hilo lilitoa taarifa nchi ya Uswidi ya kuthibitisha utekwaji nyara huo, lakini waliwataja wale waliotekwa kuwa ni wahamiaji watatu wa Kenya.

Huu ni utekaji nyara wa pili wa wafanyakazi wa misaada mwezi huu, kufuatiakutekwa kwa wafanyakazi wanne wa Baraza la Wakimbizi la Norwe. kutoka kmbi ya wakimbizi ya Dadaab nchini Kenya wiki iliyopita.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo