Julai 08, 2012
Wizara ya Kilimo, Usalama wa Chakula na Ushirika ya Tanzania, imeanzisha mpango wa utoaji risiti kwa wasambazaji wa mahitaji ya kilimo unaofanyakazi chini ya Sekta ya Mpango wa Maendeleo ya Kilimo (ASDP), gazeti la Tanzania la Daily News liliripoti hapo Jumapili (tarehe 8 Julai).
Wasambazaji wa mahitaji ya kilimo kama vile mbolea, mbegu bora na wataalamu wa ushauri sasa watahitajika kuwasilisha risiti kwa vitu walivyonunua kwa ajili ya usambazaji, kwa Maafisa Kilimo na Ufugaji wa Wilaya (DALDO) kabla ya kuwepa fedha zao, kwa mujibu wa afisa mkuu wa wizara, Michael Mayabu. Mahitaji ya risiti ni kwa ajili ya uchunguzi wa kiusalama, alisema.
Mayabu aliwaonya maafisa wa DALDO dhidi ya kuwalipa wasambazaji ambao watashindwa kuwasilisha risiti. "Ikiwa mtawalipa bila ya kupokea risiti kwanza mjue mnafanya hivyo kwa maamuzi na hasara yenu, kwa sababu ni kinyume na taratibu," alionya.
ASDP imekuwa ikifanyakazi kwa zaidi ya miaka mitatu, na imesaidia kupatikana mazao ya mahindi na mpunga mara mbili au tatu kwa kila hekta moja katika wilaya ambazo mpango huo unafanyakazi, alisema afisa mkuu wa wizara anayeshughulikia kilimo, Sarah Mlay.
Polisi nchini Tanzania wamewakamata watu 90 siku moja baada ya maandamano ambapo mtu mmoja aliuaw...
Kenya ililiomba Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa siku ya Alhamisi (tarehe 23 Mei) kufutwa kw...
Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia aliongoza sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya kuanzishwa ...
Mawaziri wa mambo ya nje wa mataifa wanachama wa Shirika la Maendeleo la Pembe ya Afrika (IGAD) w...
Kiongozi wa jamii huko Zanzibar, Mohammad Omar Said, alishambuliwa kwa tindikali siku ya Alhamisi...
Mahakama moja ya Puntland imewahukumu kifo watu saba kwa mauaji ya ulamaa wa Kisomali, Abdulkadir...
Shirika la kimataifa la misaada la Global Partnership for Education (GPE) limetangaza msaada wa d...
Shirika la kimataifa la kuteteta haki za binadamu la Amnesty International limetoa wito kwa Kenya...
Makamu wa Rais wa Kenya William Ruto ameahidi adhabu kali zaidi kwa majangili katika mswada wa Sh...
Raisi wa Kenya Uhuru Kenyatta siku ya Alhamisi (tarehe 23 Mei) alitoa majina mawili ya mwisho ya ...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji