Polisi wa Kenya wawakamata zaidi ya washukiwa 30 huko Garissa

Julai 05, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Polisi ya Kenya imewakamata zaidi ya washukiwa 30 kuhusiana na mashambulizi ya makanisa mawili huko Garissa mwishoni mwa wiki iliyopita, yaliyoua kiasi cha watu 16 na kujeruhi kwa makumi, Radio Capital FM ya Kenya iliripoti hapo Jumatano (tarehe 4 Julai).

"Tumekuwa tukichukua hatua kali na tumewakamata washukiwa kadhaa ambao wanahojiwa," alisema Naibu wa Polisi wa Mkoa wa Kaszini Mashariki Phillip Ndolo.

Kiasi cha washukiwa 20 wako kizuizini kwa mahojiano zaidi, wakati wengine waliachiwa huru kwa kukosekana ushaidi wa kutosha, CCN ilimnukuu Ndolo akisema.

Kaimu Waziri wa Usalama wa Ndani Yusuf Haji alisema maafisa 700 wa ziada wamepelekwa mjini kote na wanazunguka maeneo ili kudhibiti vitisho vya kutokuwepo na usalama kutoka kwa al-Shabaab, Capital FM iliripoti.

"Tumefanya matayarisho maalumu katika kuweka usalama na hii inajumuisha wafanyakazi zaidi wa usalama waliosambazwa," Haji alisema hapo Alhamis.

Wakati huo huo, viongozi wa Kiislamu wamesema watasaidia kuyalinda makanisa wakati wa sala, BBC iliripoti.

"Tuliamua kama hatua ya mshikamano vijana wa Kiislamu watatoa huduma za ulinzi makanisani sio tu kwa Garissa, lakini katika maeneo mengine yoyote ambako Wakristo watahisi inafaa," alisema Adan Wachu, mkuu wa Baraza Kuu la Waislamu Kenya na Baraza la Dini la Kenya.

"Haitaruhusiwa kuwa na mgawanyiko wa vikundi kama huo ndani ya nchi yetu -- yeyote atakayefanya hivyo bila shaka atashindwa," alisema.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 2)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo