Shirika la Tanzania lapokea mkopo wa nyumba za bei nafuu

Julai 03, 2012

  • 2 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na ushirika wa taaisi nane za fedha wamesaini makubaliano ya mkopo wa shilingi bilioni 165 (Dola za Kimarekani milioni 104) kwa ajili ya kujenga nyumba za bei nafuu siku ya Jumatatu (tarehe 2 Julai), gazeti la Daily News la Tanzania liliripoti.

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ya Watu, Anna Tibaijuka alisema mkataba huu "ni mkubwa kuliko yote iliyowahi kutolewa ya kuendeleza makazi nchini Tanzania".

Jumla ya benki saba za ndani, mifuko ya kijamii na taasisi nyingine za fedha ilichangia fedha katika mkopo huo.

NHC limepanga lengo la uchangiaji wa awali wa shilingi bilioni 310 (Dola za Kimarekeni milioni 196) kutekeleza mpango mkakati wake wa 2010-2015, lakini awamu hii ya kwanza italiwezesha shirika hilo la serikali kufikia lengo lake la kujenga nyumba 15,000 kabla ya mwaka 2015, alisema Mkurugenzi mkuu wa NHC Nehemia Mchechu.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 3)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • Gerald Ugho
    June 6, 2013 @ 05:57:12AM

    Napenda kujua hizi nyumba za bei nafuu ni kwa watumishi tu au?,na kama ni kwa watumishi ni utaratibu upi unatumika kumfikia muhitaji kwa wakati?,na je muhitaji anaweza kuhudumiwa popote pale Tanzania?.Kama sawa Vigezo tafadhali

  • WILSON
    February 25, 2013 @ 03:20:13AM

    ningependa kujua kua hizo nyumba za bei nafuu naweza kujengewa mahali ninapopataka mimi.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, katiba ya Kenya inapaswa kurekebishwa ili kulipa baraza jipya la Seneti madaraka zaidi?

Angalia matokeo