Julai 03, 2012
Wafanyakazi wa misaada wanne waliotekwa nyara kutoka katika kambi ya wakimbizi ya Dadaab Ijumaa waliwasili Nairobi siku ya Jumatatu (tarehe 2 Julai) baada ya kukombolewa kutoka kwa watekaji wao nchini Somalia, AFP iliripoti.
"Tunafurahi kuwa hai. Tunafurahi haya yamekwisha," alisema Quarat-UI-Ain Sadazai, Mkanada mwenye asili ya Pakstani na mmoja wa wafanyakazi waliotekwa wa Baraza la Wakimbizi la Norwe (NRC).
Sadazai, mwenye umri wa miaka 38, na wenzake -- Steven Dennis, mwenye umri wa miaka 37, ambaye pia ni Mkanada; Astrid Sehl, mwenye umri wa miaka 33, Mnorwe; na Glenn Costes, mwenye umri wa miaka 40, wa Ufilipino -- waliokolewa na kikosi cha pamoja cha Somalia na vikosi vya Kenya baada ya mapigano ya silaha ya muda mfupi ambapo mmoja wa watekaji aliuawa na washukiwa watatu walikamatwa.
Shukrani ni kwa Mungu tulizuia malengo yao ya kuwachukua mateka hawa na kuwapeleka msituni," alisema Jenerali wa Somalia Osmail Sahardid, ambaye aliongoza operesheni hiyo.
Isipokuwa kwa mtuti wa bunduki tuliweza kuwaokoa, kundi hili liliwasili Nairobi bila kudhurika.
"Tunashukuru sana kujua kuwa wenzetu wanne walipatikana na walirudishwa Kenya kwa usalama. Hii ni siku ya faraja kwetu na kwa familia za watekwaji," alisema katibu Mkuu wa NRC Elizaberth Rasmusson.
Fikra zetu za pole ziendee familia ya dereva wa NRC Abdi Ali, ambaye aliuawa wakati wa shambulio hilo Ijumaa na wafanyakzi wawili wa ndani ambao kwa sasa wanapata matibabu katika hospitali kwa majeraha yaliyotokana na tukio hilo. alisema.
Mseamaji wa NRC Rolf Vestvick alisema shirika hilo lilipunguza operesheni zake huko Dadaab mwishoni mwa wiki, lakini halitaondoa kabisa jitihada zake za misaada. "Tunamatumaini kuwa tutaweza kuendeleza kazi zetu," aliiambia televisheni ya CTV News Channel.
Wabunge wameondoa hoja yao inayomtaka Waziri Mkuu Abdi Farah Shirdon na baraza lake la mawaziri k...
Rais Ahmed Silanyo wa mkoa wa Somaliland alikutana na Mwakilishi Maalum wa Umoja wa Ulaya kwa Som...
Ukiritimba na ukosefu wa ufanisi katika bandari ya Dar es Salaam unaigharimu Tanzania na nchi jir...
Viongozi wa mkoa wa Puntland walikutana siku ya Jumanne (tarehe 21 Mei) kuwashajiisha wanawake ku...
Wanajeshi wa Somalia na wa Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia (AMISOM) waliwakamata zaidi ...
Rais Ismail Omar Guelleh wa Djibouti alijadiliana ushirikiano wa kimkakati na Kanali Saleh Ben Na...
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, vikosi vya usalama na mahakama vinapaswa kuomba radhi hadharani kut...
Waziri Mkuu wa Djibouti Abdoulkader Kamil Mohamed alitoa wito wa kuongezwa kwa ushirikiano katika...
Baadhi ya wabunge wa Somalia wameitupilia mbali hoja ya kumtaka waziri mkuu na baraza lake la maw...
Wabunge wa upinzani walidai kwamba serikali ya Tanzania imekuwa ikibana uhuru wa kujieleza na kud...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji