Juni 29, 2012
Watu wenye silaha waliua si chini ya mtu mmoja na kuteka nyara wafanyakazi wanne wa misaada katika makambi ya wakimbizi ya Dadaab nchini Kenya karibu na mpaka wa Somalia siku ya Ijumaa (tarehe 29 Juni), AFP iliripoti.
“Wafanyakazi wane wa misaada walitekwa nyara wakiwa na dereva wao, ambaye inawezekana alikuwa Mkenya,” Naibu Afisa Polisi wa Mkoa wa Kaskazini mashariki ya Kenya Philip Ndolo aliiambia AFP.
Mateka hao wanatoka Canada, Norway, Pakistani na Ufilipino, alisema.
Polisi wanawatafuta wenye silaha hao. Ambao waliondoka na mateka katika gari yao.
Maafisa wa afya wa shirika la misaada la Ujerumani GIZ alisema dereva wa Baraza la Wakimbizi la Norway (NRC) aliuwawa na askari wawili walijeruhiwa katika shambulio hilo, lililotokea katika kambi kubwa ya Ifo 2 mnamo saa za mchana.
“Mmoja wa wafanyakazi wa NRC aliuwawa, na wengine wawili walijeruhiwa,” alisema Faiysal Abdullahi, afisa wa afya wa GIZ.
Utekaji nyara ni la mwisho katika mfululizo wa mashambulizi katika kambi ya Dadaab, ambako watu wenye silaha mwezi wa Oktoba mwaka jana walitekwa Wahispania wawili waliokuwa wanafanyakazi na Madaktari Wasio na Mipaka. Bado wanashikiiwa mateka nchini Somalia.
Kambi kubwa ya Dadaab ni kambi kubwa zaidi uimwenguni, yenye wakazi zaidi ya 465,000 mpaka mwisho wa mwezi wa Mei.
Ujumbe kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya Pembe ya Afrika (IGAD) uliwatembelea maafisa mjini Mogadish...
Mshukiwa wa ugaidi na mke wake walipigwa risasi na kufa na maafisa sita wa polisi walijeruhiwa wa...
Watu watano walikamatwa siku ya Jumanne mjini Dar es Salaam wakiwa na vifaa vya kulipua katika mi...
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta aliwataka wabunge kuweka kando madai yao ya kuongezwa mishahara kwa ...
Majeshi ya serikali ya Somalia waliwaua wanamgambo tisa wa al-Shabaab wakati wa mapambanao hapo J...
Mtu asiyejulikana alimpiga kwa risasi na kumuua ofisa wa kitengo cha usalama cha kijeshi huko kas...
Muungano wa Jubilee tawala cha Kenya kilichukua uongozi wa kamati mbili muhimu za bunge Ijumaa (t...
Chama cha Wafanyabiashara na Asasi ya Chakula na Kilimo ya Umoja wa Mataifa vinatoa mafunzo kwa w...
Balozi wa Umoja wa nchi za Ulaya nchini Tanzania Filiberto Ceriani Sebregondi aliwahamiza waandis...
Makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto, alisema kazi za Misheni ya Umoja wa Afrika nchini Somalia ...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji
Maoni ya msomaji
Makafiri al-Shabaab wameanza kuvunjika. Mungu ni Mkubwa.