Ujenzi wa bomba la gesi la Tanzania kuanza karibuni

Juni 28, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Wafanyakazi wa serikali ya Tanzania wamekwenda nchini China kusaini makubaliano ya mkopo wa dola bilioni 1.2 na benki ya Usafirishaji na Uingizaji ya nchi hiyo, liliripoti gazeti la Tanzania la Daily News hapo Alhamis (Juni 28).

Mkopo huo utagharamikia ujenzi wa bomba la gesi asilia lenye urefu wa kilomita 532 baina ya Mnazi Bay , Mtwara na Dar es Salaam . Mradi huo utajenga bomba jipya la inchi 24 hadi 36 kati ya Mnazi Bay na Somanga na kutanua bomba lililopo sasa kati ya Somanga na Dar es Salaam kutoka inchi 16 hadi 36. Bomba hilo litaongeza mara mbili uwezo wake kwa kusafirisha gesi yenye mita za ujazo milioni 210 kwa siku.

“Tunatarajia mradi huu utaanza wakati wowote kutoka sasa kwani tayari tumeshapata fedha,” alisema mwenyekiti wa Shirika la Maendeleo ya Mafuta la Tanzania , Michael Mwanda.

Gesi asilia inatoa asilimia 35 ya umeme nchini humo, kwa mujibu wa gazeti la Daily News.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 5)

Dislike_icon(1)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo