Juni 25, 2012
Kampuni ya uhandisi ya Kijerumani imetia saini mkataba wa kujenga kinu cha umeme cha megawati 95 katika mji wa Kenya wa Thika, gazeti la Business Daily la Kenya liliripoti hapo Jumapili (tarehe 24 Juni).
Kampuni ya MAN Diesel & Turbo, tawi la Volkswagen AG, litajenga kinu cha umeme cha dizeli chenye thamani ya shilingi bilioni 12 (dola za Kimarekani milioni 143). Kampuni hiyo ilitia saini mkataba pamoja na mwenye mradi huo, Kampuni ya Thika Power Limited, kitengo cha kampuni ya Matelec Group cha Lebanon.
Kinu hicho kinatarajiwa kuzalisha megawati 88 za umeme na joto linalopotea kutoka injini hizo zitatumika katika bomba ya mvuke ili kutoa megawati 6.8 zaidi za umeme. Umeme utakaozalishwa katika kinu hicho utauzwa kwa kampuni ya Kenya Power ili kuingizwa katika gridi ya taifa.
MAN Diesel & Turbo tayari imeanza kazi katika ujenzi huo, ambao unatarajiwa kuzalisha umeme mwaka ujao.
Polisi nchini Tanzania wamewakamata watu 90 siku moja baada ya maandamano ambapo mtu mmoja aliuaw...
Kenya ililiomba Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa siku ya Alhamisi (tarehe 23 Mei) kufutwa kw...
Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia aliongoza sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya kuanzishwa ...
Mawaziri wa mambo ya nje wa mataifa wanachama wa Shirika la Maendeleo la Pembe ya Afrika (IGAD) w...
Kiongozi wa jamii huko Zanzibar, Mohammad Omar Said, alishambuliwa kwa tindikali siku ya Alhamisi...
Mahakama moja ya Puntland imewahukumu kifo watu saba kwa mauaji ya ulamaa wa Kisomali, Abdulkadir...
Shirika la kimataifa la misaada la Global Partnership for Education (GPE) limetangaza msaada wa d...
Shirika la kimataifa la kuteteta haki za binadamu la Amnesty International limetoa wito kwa Kenya...
Makamu wa Rais wa Kenya William Ruto ameahidi adhabu kali zaidi kwa majangili katika mswada wa Sh...
Raisi wa Kenya Uhuru Kenyatta siku ya Alhamisi (tarehe 23 Mei) alitoa majina mawili ya mwisho ya ...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji