Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa laisifu Tanzania kwa juhudi zake

Juni 25, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) imeisifu Tanzania kwa kuwapatia makazi wakimbizi kutoka ukanda huo na kuimarisha amani na utulivu, gazeti la The Guardian la Tanzania liliripoti siku ya Jumatatu (tarehe 25 Juni).

Mkabala wa serikali wa kushughulikia changamoto zinazoletwa na wakimbizi zimesaidia kupunguza idadi ya wakimbizi nchini Tanzania kufikia 134,940, huku 500,000 wakiwa wamerejea makwao, kaimu mwakilishi wa UNHCR nchini Chansa Kapaya alisema katika maadhimisho ya Siku ya Wakimbizi Duniani mjini Dar es Salaam wiki iliyopita.

Kapaya aliusifu uamuzi wa serikali wa mwaka 2010 wa kuwapa uraia wakimbizi 162,000 wa Burundi waliokuwa wameishi Tanzania kwa zaidi ya miaka 40.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon alisisitiza umuhimu wa nchi kuwapatia hifadhi wasiokuwa na makazi.

"Ni lazima tufanye kazi kwa pamoja ili kuhamasisha dhamira ya kisiasa na uongozi kuzuia na kukomesha migogoro inayoleta mtiririko wa wakimbizi," alisema. "Mahali pa kurejesha usalama, ni lazima tukabiliane na vyanzo vya msingi vya mgogoro, ili kurahisisha urejeshwaji endelevu wa wakimbizi kwa kuwapatia maisha mazuri, huduma na utawala wa sheria."

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo