Vikundi vya Waislamu Kenya vyaunga mkono mswada wa kuzuia ugaidi

Juni 25, 2012

  • 1 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Bunge la Kenya litaanzisha sheria mpya ya kupinga ugaidi katika wiki zijazo ambayo itawafunga maisha gerezani watu watakaohusika katika matukio ya ugaidi, Redio Capital FM iliripoti siku ya Jumapili (tarehe 24 Juni).

Mswada wa Kuzuia Ugaidi wa mwaka 2012 ulianzishwa awali mwaka 2003 na baadaye ulifutwa baada ya fujo zilizosababishwa na baadhi ya vifungu vilivyopingwa na baadhi ya vikundi vya Kiislamu.

Lakini mwenyekiti wa Muunganiko wa Taasisi za Kiislamu Sheikh Athman Mponda alisema taasisi inaunga mkono mswada mpya na kuikana dhana kwamba ni moja ya njia ya kukandamiza Uislamu.

"Tuanaunga mkono mswada, tumeupitia na umezingatia nyanja zote. Hauna ubaguzi kwa jamii ya Kiislamu," Mponda aliwaeleza waandishi wa habari huko Nairobi.

Mponda alisisitiza kuwa dini haina maana kubwa katika vurugu inayoendelea huko Somalia.

"Tumesikia vijana wengi wa kiume wakisafiri kuelekea Somalia kupigana kile wanachokiita vita vya kidini. "Kwa nini wajihusishe katika vita na kudai kwamba wanajiunga na vita vya kidini? Hakuna mahali popote katika Qur'an palipoeleza kwamba mtu anaweza kumuua mtu mwingine au kujiua mwenyewe, kwa hivyo kwa nini watu wajihusishe na mabomu ya kujitoa muhanga?"

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • kenyanpatriot
    June 26, 2012 @ 06:50:40AM

    Sijawahi kusikia kikundi hiki kinaonekana kuwa ni msemaji wa serikali ili kuhalalisha matendo yake.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo