Serikali ya Somalia kupanua mapambano dhidi ya al-Shabaab

Juni 25, 2012

  • 1 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Jeshi la Somalia litaongeza operesheni dhidi ya al-Shabaab nchini kote, Waziri wa Ulinzi Hussein Arab Isse alisema Jumatatu (tarehe 25 Juni).

Akiandamana na Kamanda wa jeshi la Somalia Abdulqadir Sheikh Ali Dini, Isse alikagua kambi za jeshi huko Mogadishu siku ya Jumapili na kupata maelezo kuhusu hali ya mafunzo, Shirika la Habari la Taifa liripoti. Waziri alisema alipata moyo kuwaona wanajeshi wa Somalia wakiwa tayari kuitetea nchi yao na kuwa tayari kufundishwa nchini.

Isse aliwapongeza wanajeshi wa Somalia na wanajeshi wa Umoja wa Afrika kwa maendeleo waliyoyafikia hadi sasa na kurudia kusema uwajibikaji wa serikali katika kuwaondoa al-Shabaab kutoka Somalia ya Kusini na ya Kati ili kurejesha amri na amani nchini, haya yalielezwa na Mtandao wa Shabelle Media Network ya Somalia.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 1)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • Muhamad
    June 26, 2012 @ 10:54:48AM

    Al-Shabaab wako katika ukingo wa kushindwa na kuangamizwa kwao kutaleta matumaini kwa Somalia. Kwa miongo sasa nchi hii imekuwa ikipambana na umasikini na vita vya wenyewe kwa wenyewe na sasa ni wakati wa kunyanyuka kutokana na yote hayo. Sasa, ni kwa namna gani kushindwa kwa al-Shabaab kunaweza kusaidia kuijenga Somalia? Sote tunajua kuwa wawekezaji wawe au ndani au wa nje wanadhamana katika kuchangia maendeleo ya nchi. Kutokana na al-Shabaab kwisha ondoka, wawekezaji wengi watakuwa na imani ya kuwekeza pesa zao nchini. Kuangamizwa kwa al-Shabaab pia kutawawezesha wenyeji kujihusisha na shughuli za kujipatia fedha na kuimarisha uchumi wao. Wakimbizi wote hawa ambao wamekimbia kwa sababu ya vita watarejea na kujiunga na wengine katika kujenga taifa lao. Wakati tishio la al-Shabaab litapokuwa limeondolewa wafadhili watakuwa na imani na wataisaidia Somalia kukua katika masuala ya miundombinu na kuimarisha hali za maisha. Watu watakuwa na imani zaidi na kufanyakazi kuelekea lengo moja ambalo ni kuijenga Somalia.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo