Mlipuko wa Mombasa waua 3 na kujeruhi dazeni; mshukiwa mmoja ashikiliwa

Juni 25, 2012

  • 3 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Shambulio la bomu katika baa mji wa bandari wa Mombasa huko Kenya Jumapili (tarehe 24 Juni) liliua watu watatu na kujeruhi 30, kwa mujibu wa Shirika la Msalaba Mwekundu Kenya na maofisa wa polisi.

Waathirika walipelekwa katika hospitali iliyo karibu wakati polisi na kitengo dhidi ya ugaidi na uchunguzi wa uhalifu kikianza ukaguzi katika eneo hilo, gazeti la Daily Nation la Kenya liliripoti.

Mlipuko ulitokea Jericho Beer Garden katika Wilaya ya Mishomoroni, ambapo mashabiki wa mpira wa miguu walikuwa wakiangalia mechi ya robo fainali ya Euro 2012 kati ya Uingereza na Italia, AFP iliripoti.

“Waathirika wawili walifariki wakiwa hospitalini. Mmoja alifariki kabla katika eneo la tukio,” alisema msemaji wa Shirika la Msalaba Mwekundu Kenya Nelly Muluka.

Mkuu wa Polisi wa Jimbo Aggrey Adoli alisema mmoja wa waliojeruhiwa anashikiliwa kama mshukiwa. Mmoja kati ya watu waliojeruhiwa anatusaidia kwa sababu alitoa kauli ya kuchanganya,” alisema.

Hakuna kundi lililodai kuhusika na shambulio hilo.

Kenya imekuwa ikishuhudia mashambulio kadhaa ya kigaidi toka ilipozindua kampeni ya kijeshi dhidi ya al-Shabaab katika nchi jirani ya Somalia mwaka uliopita, ikiwa ni pamoja na shambulio la mgahawa wa Mombasa mwezi Mei.

Mlipuko wa Jumapili umekuja baada ya serikali ya Marekani kutoa tahadhari ya tishio la shambulio la kigaidi lililo karibu kutokea huko Mombasa.” Ubalozi wa Ufaransa huko Nairobi pia ulitahadharisha raia kuwa waangalifu sana,” huko Mombasa na maeneo yanayozunguka eneo hilo.

Tahadhari hiyo imekuja baada ya polisi wa Kenya kusema kuwa imewashikilia raia wawili wa Irani Jumatano na Alhamisi kuhusiana na kushukiwa kuwa na uhusiano na mtandao wa kigaidi unaopanga kulipua mabomu Mombasa na Nairobi, AFP iliripoti.

Mkuu wa Uchunguzi wa Uhalifu Ambrose Munyasia alisema polisi wa jimbo la Pwani walikuwa katika "tahadhari kubwa”.

“Tutafanya kila linalowezekana kuhakikisha watu katika Pwani wako salama,” alisema Jumamosi. “Tumeimarisha usalama lakini tunatoa wito kwa wananchi kufanya kazi kwa karibu na sisi katika kutupa taarifa.”

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 3)

Dislike_icon(2)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • helly
    June 27, 2012 @ 07:07:46AM

    Napenda

  • Ali
    June 26, 2012 @ 12:57:47PM

    Oh Mwenyezi Mungu, mpaka lini wahalifu hawa watashambulia watu!!!! Mwenyezi Mungu atawasaidia watu na watawashinda magaidi kwa uhakika, hili ni suala la wakati tu.

  • jeremiah jeremy
    June 26, 2012 @ 01:51:54AM

    NSIS imelala kabisa. Inakuwaje kuwa tahadhari imetolewa na watu wa nje wakati NSIS hawana habari na baadaye shambulio linatokea kama ilivyoelezwa kabla, ikiwa wao hawakuwa wamelala?

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo