Aina uadimifu ya pundamilia waogofya kwa uchungaji ovyo

Juni 21, 2012

  • 2 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Idadi ya aina uadimufu ya pundamilia wajulikanao kama Grevy inapungua kwa sababu ya ugombaniaji wa maeneo ya kuchunga mifugo nchini Kenya, liliripoti shirika la habari la AFP hapo Alhamis (tarehe 21 Juni).

Kupotea kwa aina za viumbe hao kunakochangiwa na kuongezeka kwa idadi ya watu, uwindaji na maradhi kunamaanisha kwamba ni pundamilia wachache chini ya 2,500 waliobakia, ikilinganishwa na 15,000 waliokuwepo mwaka 1970.

Eneo la hifadhi ya wanyama la West Gate katika mbuga za Naibelibeli nchini Kenya lilikuwa nyumbani kwa aina ya pundamilia ya Grevy 500 wakati mmoja, lakini ziara ya karibuni ya wataalamu wa wanyamapori imegundua kwamba wamebakia watano tu. Pundamilia wa Grevy wanaotambuliwa kwa masikio yao marefu na michoro tofauti na pundamilia wa kawaida, walikuwa wakionekana katika maeneo ya Somalia, Djibouti, Eritrea, Kenya na Ethiopia, lakini sasa wanaonekana Kenya na Ethiopia tu.

“Watu wanajikalia na kujichungia wanyama kila mahala,” alisema Peter Lalampaa kutoka kabila la Samburu na meneja mwandamizi wa mfuko wa Pundamilia wa Grevy, ambaye aliitembelea hifadhi ya wanyama ya West Gate. “Shule zinajengwa kwa wingi hapa na wachungaji waliozoea kurandaranda sasa wamekaa mahala mamoja, kwa hivyo uchungaji wa papo kwa papo limekuwa tatizo.”

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • عمر خالد
    August 9, 2012 @ 04:24:07PM

    Nadhani hakuna maisha mazuri zaidi ya maisha ya utulivu na kazi itokanayo na kilimo, na tutafaidika sana ikiwa tutafanikiwa kuivutia jamii ya wafugaji kufanyakazi katika sekta ya kilimo na kulima mashamba na kufuga mifugo. Hili ndilo tunalotaka, kwa sababu hatua hii chanya itakua hatua kubwa kwa kiwango cha uchumi. Ili kufikia hatua hii, serikali lazima iwaunge mkono na kuiitia moyo sekta ya kilimo kwa kupeana mahitaji yote ya wakulima, na kuwafanya wajihisi kuwa inawashughulikia wao na ardhi yao na kwamba itawapatia mahitaji yanayohitajika na kununua mazao yao, pamoja na kushughulikia matatizo mengine ambayo sekta ya kilimo imeshuhudia hivi karibuni.

  • ngugi
    June 22, 2012 @ 04:41:26AM

    Mnahitajika kuweka picha katika machapisho yenu.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo