Makampuni ya Kifaransa ‘tayari kuwekeza’ Tanzania

Juni 21, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Makampuni kutoka Ufaransa yanajitayarisha kuwekeza nchini Tanzania, alisema mwanadiplomasia wa ngazi za juu wa Kifaransa hapo Jumanne (tarehe 19 Juni).

“Licha ya baadhi ya changamoto, uchumi wa Tanzania unakuwa…katika maeneo ya biashara, uwekezaji, na kadhalika.” Mkurugenzi Mkuu anayehusika na masuala ya Afrika wa Ufaransa Elisabeth Barbier aliliambia gazeti la The Guardian la Tanzania. "Makampuni ya Ufaransa yako tayari kuwekeza nchini Tanzania. Wanataka kunufaishwa na uwezo wa ukuaji na maendeleo uliopo."

Alisema uwezo wa kuwekeza nchini Tanzania unatakiwa kutumiwa vyema ili kutoa matokeo mazuri katika kiwango cha umma, kama vile kuinua hali ya maisha ya wananchi.

Barbier pia alibainisha kuwa Umoja wa nchi za Ulaya unampango kuwa mbia na Tanzania na nchi nyingine za Afrika ili kupambana na maharamia.

“Katika kiwango cha Umoja wa nchi za Ulaya kuna mradi maalum ambao utaanza hivi karibuni kujenga uwezo wa baadhi ya nchi za Afrika, Tanzania ikiwa mojawapo, kupambana na wimbi linaloongezeka la maharamia kwenye Bahari ya Hindi,” alisema.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo