Umoja wa Mataifa wajitolea kuwasaidia wakimbizi wa Somalia

Juni 21, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) linaendelea kujitolea kuwasaidia wakimbizi wa Somalia, msemaji wa shirika hilo, Adrian Edwards, aliliambia gazeti la Kulmiye News la Somalia hapo Jumatano (tarehe 20 Juni).

Edwards alisema UNHCR inaendelea kuwahudumia wakimbizi wa Kisomali nchini Kenya, Uganda, Ethiopia, Djibouti na Misri.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon, pia alisisitiza ulazima wa hali ya wakimbizi wa Somalia hapo Jumatano katika Siku ya Wakimbizi Duniani, akitaja kwamba makambi ya wakimbizi ya Dadaab ni mji wa tatu kwa ukubwa nchini Kenya ukiwahifadhi Wasomali 500,000. “Nchi zinazowahifadhi wakimbizi hazipaswi kuachiwa mzigo huu peke yao”, alisema.

“Ni lazima tufanye kazi pamoja kuhamasisha dhamira ya kisiasa na uongozi kuzuia na kumaliza migogoro inayopeleka wakimbizi kumiminika sehemu nyingine,” alisema Ban. “Pale usalama unaporudishwa, lazima tutatue mambo yanayosababisha migogoro, kuruhusu kurudi kwa wakimbizi nyumbani kupitia upatikanaji wa maisha, huduma, na utawala wa sheria.”

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 1)

Dislike_icon(1)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, katiba ya Kenya inapaswa kurekebishwa ili kulipa baraza jipya la Seneti madaraka zaidi?

Angalia matokeo