Ukombozi wa Afmadow wanyanyua biashara

Juni 21, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Hali ya maisha mjini Afmadow imeimarika na biashara kurudi katika hali ya kawaida baada ya vikosi vya Somalia na Kenya kuwaondoa wapiganaji wa al-Shabaab kutoka kwenye mji huo wiki tatu zilizopita, liliripoti gazeti la The Standard la Kenya hapo Jumatano (tarehe 20 Juni).

Biashara zimerudi katika masoko ya mji huo, huku wafanyabiashara wakiuza mazao kutoka mashambani, vyakula vya mifuko na makopo, nguo na bidhaa nyingine. Hata hivyo, mji umeendelea kukosa maji na umeme.

Juu ya hayo, kituo kikuu cha polisi mjini humo kimefanyiwa matengenezo na wakaazi wanajihisi salama kutembea kwa miguu hadi nyakati za usiku, kwa mujibu wa gazeti hilo la The Standard.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 2)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo