Bunge la Kenya latafuta njia za kuongeza usalama kabla ya uchaguzi

Juni 21, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Kamati ya Bunge la Kenya lilisema shilingi bilioni 83.5 (dola bilioni 1) zilizotengwa kwa usalama katika bajeti ya mwaka 2012-2013 hazitoshi.

Fedha zilizotengwa kwa usalama wa taifa hazitoshi, kutokana na vitisho vingi vinavyoikabili nchi kwa sasa,” Fred Kapondi, mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya utawala na usalama wa taifa, alisema hapo Jumatano (tarehe 20 Juni) katika Redio Milele ya Kenya.

Ingawa serikali hapo Aprili ilitangaza mpango wa kuajiri maafisa wapya 7,000 kuelekea uchaguzi ujao, pesa zilizotolewa ni kwa maafisa 3,500 tu, gazeti la Daily Nation la Kenya liliripoti.

Ili kuongeza usalama, serikali inachukua hatua za kupunguza uwepo wa silaha za moto, ikiwa ni pamoja na kurekebisha Muswada wa Silaha za Moto ili kutoa adhabu kali kwa umiliki wake usio halali, gazeti la The Standard la Kenya liliripoti.

Ripoti ya Silaha Ndogondogo iliyotolewa Jumatano inasema kuna kiasi cha silaha za moto haramu 680,000 nchini Kenya.

"Silaha hizi zimetapakaa kila sehemu lakini tunatumaini kuchukua hatua za kukabiliana na usumbufu mbele ya uchaguzi," alisema Mutea Iringo Katiba wa Kudumu ya Wizara ya Usalama wa Ndani.

Iringo alisema mzozo na al-Shabaab nchini Somalia umezidisha kuenea kwa silaha haramu. “Tuna matumaini kuwa operesheni nchini Somalia italeta busara hatimaye kwa sababu huu ndio chanzo kikuu cha tatizo hili,” alisema.

Iwapo sheria zitarekebishwa, wamiliki wa bunduki haramu watafungwa kifungo cha maisha, ambapo adhabu kubwa kwa sasa nikifungo cha miaka 15, kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 1)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo

Nyenzo