Wanandoa wa Afrika ya Kusini waliotekwa nyara Somalia waachiwa huru

Juni 21, 2012

  • 1 Maoni
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Vikosi vya usalama vya Somalia vimewaokoa wanandoa kutoka Afrika ya Kusini ambao walitekwa nyara katika Bahari ya Hindi na kuzuiliwa kwa muda wa miezi 18, Waziri wa Ulinzi wa Somalia Hussein Arab Isse alisema hapo Alhamisi (tarehe 21 Juni).

“Uokozi ulianza usiku uliopita (wa Jumatano) na ulidumu mpaka asubuhi hii na mnaweza kuona kuwa wanandoa waliokolewa salama,” Isse alisema wakati wa mkutano na waandishi wa habari akiwa pamoja na wanandoa hao, Debbie Calitz na Bruno Pelizzari.

Isse alisema uvamizi huo ulikuwa ni operesheni ya pamoja baina ya vikosi vya usalama na jeshi na kwamba wanandoa wamekomolewa kutoka kwa “waasi wenye uhusiano na al-Qaeda”, kwa mujibu wa AFP.

Calitz and Pelizzari walikuwa wakisafiri katika Bahari ya Hindi nje ya mwambao wa Kenya mwaka 2010 ambapo boti yao ya kifahari ilipotekwa nyara na maharamia 12 walioipelea Somalia na kuwachukua wanandoa huko Barawe.

Afrika ya Kusini ilikaribisha habari za kuokolewa kwa wanandoa hao na kuwashukuru watu wote waliohusika katika operesheni.

“Serikali ya Afrika ya Kusini inataka kuelezea shukurani zake za dhati kwa Serikali ya Mpito ya Shirikisho ya Somalia kufuatia kwa kuachiwa huru kwao hapo Jumatano,” Waziri wa Mambo ya Nje alisema katika taarifa. “Wanandoa wako katika afya njema na wana hamu ya kuungana na wapendwa wao.”

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 6)

Dislike_icon(1)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Maoni ya msomaji

  • Adriana Stuijt
    June 22, 2012 @ 01:52:00AM

    Wanandoa hawa walikuwa sehemu ya mabaharia katika boti ya fahari iliyokuwa ikielekea Richards Bay Afrika ya Kusini - na ambayo ilitekwa nyara nje ya mwambo wa Tanzania. Hata hivyo kepteni wa Afrika ya Kusini wa boti ndogo aliokolewa na meli ya jeshi la majini la Uholanzi iliyokuwa inawafukuza maharamia wakati ule, na maharamia watano walikamatwa na kushitakiwa katika mahakama ya sheria ya Uholanzi, ambapo Waholanzi waliweza pia kumuokoa kepteni. Hata hivyo wanandoa hawa wa Africaans - ambao ni daraja la wafanyakazi masikini - walizuiwa kwa mtutu wa bunduki na maharamia waliobaki waliokuwa wakikimbia - kwa hivyo kushindwa kukimbia. Hii ilipelekea kukamatwa kwao. Shukrani nyingi kwa watu wa somalia kwa njia yao ya ubinadamu ya kushughulikia opresheni hii ya kuwaokoa wanandoa masikini kifedha ambao familia zao zilikuwa zikijaribu kwa kukata tamaa ili kukusanya fedha za kikomboleo.

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo