Mawaziri wa Somalia wafanya mkutano maalumu kuhusu vizuizi vya barabara visivyo halali

Juni 20, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Baraza la Mawaziri la Somalia lilifanya mkutano wiki hii kujadili vizuizi vya barabara visivyo halali ambavyo vimeanzishwa Mogadishu yote kwa miongo miwili iliyopita, Mtandao wa habari wa Shabelle wa Somalia uliripoti Jumanne (tarehe 19 Juni).

Waziri wa habari, Posta na Mawasiliano Abdulkadir Hussein Mohamed alisema baraza la mawaziri kwa pamoja lilikubaliana “kuchukua hatua kali dhidi ya vituo vya ukaguzi visivyo halali vinavyosumbua Mogadishu na vijiji vya jirani chini ya udhibiti wa Serikali ya Mpito ya Shirikisho.”

Waziri pia alisema Waziri Mkuu Abdiweli Mohammed Ali amekuwa akikutana na mashirika ya ulinzi ya taifa na wakazi wa Mogadishu kujadili vizuizi vya barabarani.

Waendesha pikipiki wamelalamika kwamba watu wenye silaha waliovaa sare za serikali wanadai fedha kwa nguvu katika vituo vya ukaguzi.

Vikosi vya serikali ya Somalia huko Mogadishu hivi karibuni vilirushiana risasi na watu wenye silaha waliovaa sare za jeshi, Shabelle iliripoti Jumanne.

Mkuu wa Polisi wa wilaya ya Hodan Hassan Mohammed Abukar alisema mapigano yaliendelea baada ya vikosi vya ulinzi kuwavamia watu wenye silaha ambao walikuwa wakichukua fedha kinyume cha sheria katika kituo cha ukaguzi.

"Vikosi vya ulinzi vimemkamata mmoja wa genge la wahalifu wakati wa operesheni na kumkabidhi kwa mahakama ya kijeshi ya Somalia ili sheria ichukue mkondo wake kutokana na kujihusisha kwake katika kuwapora raia huko Mogadishu,” Abubakar alisema.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 1)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo