Dar es Salaam kuandaa mashindano ya mpira wa miguu ya kanda

Juni 17, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Baraza la Vyama vya Mpira vya Afrika ya Mashariki na Kati (CECAFA) limesogeza tarehe ya mashindano ya Kombe la Kagame kufanyika Dar es Salaam kuwa tarehe 14 Julai, Katibu Mkuu wa CECAFA Nicholas Musonye alisema hapo Jumamosi (tarehe 16 Juni).

Michezo hiyo iliahirishwa kutokana na matatizo ya kifedha, gazeti la The Citizen la Tanzania liliripoti. “Tumeziendea taasisi kadhaa kwa ajili ya msaada wa kifedha, lakini hakuna hata moja ambayo imetupa jibu la matumaini,” Musonye alisema.

Mlezi wa kombe hilo Paul Kagame ametoa zawadi ya fedha kwa mashindano hayo, na CECAFA imo katika mchakato wa kukusanya misaada zaidi.

Hii ni mara ya tatu mfululizo kwa mashindao hayo kufanyika Tanzania. Timu kutoka Afrika zitashiriki katika mashindano hayo.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 0)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo