Benki ya Kenya yaangalia kuwekeza nchini Somalia

Juni 13, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Equity Bank inafikiria kupanua biashara yake ya kanda ndani ya Somalia ili kutoa fursa kwa wawekezaji wa Kenya, gazeti la Africa Review liliripoti Jumanne (tarehe 12 Juni).

“Pesa ya kodi ya Wakenya imekuwa ikitumika katika kuikomboa na kuleta amani katika nchi ile,” alisema afisa mtendaji wa Equity Bank James Mwangi wakati wa chai ya asubuhi mjini Nairobi hapo Jumatatu ili kusherehekea zawadi yake ya Ernst & Young World Entrepreneur kwa mwaka 2012.

“Sasa tunatafuta sehemu ya gawio na hili linawezekana tu kwa kuwekeza katika soko,” Mwangi alisema.

Equity Bank inafanyakazi Kenya, Rwanda, South Sudan, Tanzania na Uganda.

Jeshi la Ulinzi la Kenya liliingia Somalia ili kupambana na al-Shabaab hapo Oktoba, na majeshi yake 4,631 yalijiunga rasmi na AMISOM mwanzoni mwa mwezi huu.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 2)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo