Juni 12, 2012
Viongozi wanaendesha msako mkubwa wa watu ili kuwapata watu wawili wenye bunduki waliojaribu kumuua hakimu wa eneo hilo, Waziri wa mambo ya Ndani Duur Arale alisema katika mkutano na waandishi wa habari huko Hargeisa hapo Jumatatu (tarehe 11 Juni).
Watu wenye bunduki walipiga risasi Hakimu Abdirashid Mohamed Duran siku ya Jumatatu asubuhi, vyombo vya habari vya Somaliland viliripoti. Moja ya risasi ilimpata Duran, ambaye alipelekwa katika hospitali ya Djibouti wa matibabu.
Arale aliwaambia waandishi wa habari kuwa jaribio hilo la mauaji lilikuwa mbinu rahisi iliyokusudiwa kukwamisha usalama na utulivu katika eneo hilo. Aliahidi kukamatwa kwa watu hao wenye silaha, wakati wachunguzi wa polisi wanawatafuta wahusika.
“Serikali sio tu inaahidi usalama lakini pia huduma kama kawaida,” Arale alisema, na kuwataka wananchi kuwa walinzi kuhusu vitisho vya usalama.
Hakimu Duran karibuni alihusika katika kesi ya kuwahukumu maafisa watatu wa serikali na viongozi wawili wa ndani kwa kuhusika kwao katika kujipatia isivyo halali chakula cha msaada.
Polisi nchini Tanzania wamewakamata watu 90 siku moja baada ya maandamano ambapo mtu mmoja aliuaw...
Kenya ililiomba Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa siku ya Alhamisi (tarehe 23 Mei) kufutwa kw...
Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia aliongoza sherehe za maadhimisho ya miaka 50 ya kuanzishwa ...
Mawaziri wa mambo ya nje wa mataifa wanachama wa Shirika la Maendeleo la Pembe ya Afrika (IGAD) w...
Kiongozi wa jamii huko Zanzibar, Mohammad Omar Said, alishambuliwa kwa tindikali siku ya Alhamisi...
Mahakama moja ya Puntland imewahukumu kifo watu saba kwa mauaji ya ulamaa wa Kisomali, Abdulkadir...
Shirika la kimataifa la misaada la Global Partnership for Education (GPE) limetangaza msaada wa d...
Shirika la kimataifa la kuteteta haki za binadamu la Amnesty International limetoa wito kwa Kenya...
Makamu wa Rais wa Kenya William Ruto ameahidi adhabu kali zaidi kwa majangili katika mswada wa Sh...
Raisi wa Kenya Uhuru Kenyatta siku ya Alhamisi (tarehe 23 Mei) alitoa majina mawili ya mwisho ya ...
(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji