Viongozi wa Somaliland wawasaka washukiwa wa mauaji

Juni 12, 2012

  • + Toa maoni sasa
  • Chapisha
  • Panga upya Punguza Ongeza

Viongozi wanaendesha msako mkubwa wa watu ili kuwapata watu wawili wenye bunduki waliojaribu kumuua hakimu wa eneo hilo, Waziri wa mambo ya Ndani Duur Arale alisema katika mkutano na waandishi wa habari huko Hargeisa hapo Jumatatu (tarehe 11 Juni).

Watu wenye bunduki walipiga risasi Hakimu Abdirashid Mohamed Duran siku ya Jumatatu asubuhi, vyombo vya habari vya Somaliland viliripoti. Moja ya risasi ilimpata Duran, ambaye alipelekwa katika hospitali ya Djibouti wa matibabu.

Arale aliwaambia waandishi wa habari kuwa jaribio hilo la mauaji lilikuwa mbinu rahisi iliyokusudiwa kukwamisha usalama na utulivu katika eneo hilo. Aliahidi kukamatwa kwa watu hao wenye silaha, wakati wachunguzi wa polisi wanawatafuta wahusika.

“Serikali sio tu inaahidi usalama lakini pia huduma kama kawaida,” Arale alisema, na kuwataka wananchi kuwa walinzi kuhusu vitisho vya usalama.

Hakimu Duran karibuni alihusika katika kesi ya kuwahukumu maafisa watatu wa serikali na viongozi wawili wa ndani kwa kuhusika kwao katika kujipatia isivyo halali chakula cha msaada.

Unaonaje kuhusu makala hii? (Jumla ya Kura 1)

Dislike_icon(0)

(Sera za kutoa Maoni) *Inaonesha Maeneo yanayohitaji

Habari Mpya kabisa

Katika Mwangaza

Jisajili

Kura

Je, unadhania kupigwa marufuku kwa hotuba ya chuki na Tanzania kutakomesha mashambulizi dhidi ya makanisa na misikiti?

Angalia matokeo